• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SHEREHE ZA BULABO KUPANDISHWA HADHI KUWA URITHI WA UTAMADUNI

Posted on: June 21st, 2025

SHEREHE ZA BULABO KUPANDISHWA HADHI KUWA URITHI WA UTAMADUNI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Chifu Mkuu Hangaya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa serikali imeamua kuboresha tamasha la Bulabo kuwa la Urithi wa Utamaduni usioshikika na kwamba Wizara ya Utamaduni inakamilisha taratibu ili kufikia malengo hayo.

Mhe. Dkt. Samia ameeeleza hayo leo tarehe 21 Juni, 2025 wakati akifungua tamasha la utamaduni wa Wasukuma (Bulabo) la kanda ya ziwa lililofanyika katika Viwanja vya Red Cross Bujora – Kisesa wilayani Magu na amesisitiza jamii kuenzi na kulinda utamaduni kwa maslahi ya sasa na vizazi vijavyo.

“Hakika nimeshuhudia mambo mazuri sana ya kihistoria, hongera kwa kujenga taifa lenye maadili nawapongeza sana kwa kudumisha utamaduni lakini niendelee kusisitiza kulinda kikamilifu silka na mila zetu na tuache kuiga mila za kigeni zinazoweza kuharibu amani yetu.” Dkt. Samia.

Aidha, kuelekea kipindi cha uchaguzi amewataka waganga kutofanya ramli chonganishi kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi nchini ili kuendelea kulinda uhai na utu wa watu wa makundi yote.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema serikali imejiridhisha  na uendeshaji wa sherehe za mavuno ya bulabo zinazotunza mila zikiwa zimeunganishwa na Ekaristi Takatifu ya Kanisa Katoriki ambapo Wizara ipo katika hatua za mwisho kulifanya Tamasha hilo kuwa Urithi wa Utamaduni usioshikika wa dunia chini ya UNESCO.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema tamasha hilo limelenga kuhamasisha utunzaji wa mazingira, kulinda tamaduni na wananchi kushiriki uchaguzi Mkuu wa 2025 na kwamba Mwanza kuna wapiga kura wapya zaidi ya laki tano kutoka kwenye waliopiga kwenye uchaguzi uliopita Milioni 1.8.

Naye Baba Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoriki la Mwanza, Mhashamu Renatus Nkwande amemshukuru Rais Samia kwa kutambua nafasi ya utamaduni na kuruhusu utoaji wa vibali kwa ajili ya kumiliki nyala za serikali katika kituo cha Bujora ili kukipatia uhai na kuleta taswira halisi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMA TUNAHITAJI KUSONGA MBELE NI LAZIMA KUJIUNGA NA USHIRIKA – RAS BALANDYA

    June 24, 2025
  • RAS BALANDYA AFUNGUA MAFUNZO YA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA

    June 23, 2025
  • SHEREHE ZA BULABO KUPANDISHWA HADHI KUWA URITHI WA UTAMADUNI

    June 21, 2025
  • SUNGUSUNGU DAY YAFANA MWANZA, RAIS SAMIA ASIMIKWA UTEMI

    June 20, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.