• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

STORI YA BABA NA WATOTO WATATU WALIOKUMBWA NA UGONJWA WA KUTETEMEKA NA KUPOOZA MWILI YAMGUSA RC MTANDA

Posted on: February 12th, 2025

STORI YA BABA NA WATOTO WATATU WALIOKUMBWA NA UGONJWA WA KUTETEMEKA NA KUPOOZA MWILI YAMGUSA RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Februari 12, 2025 amefika katika Mtaa wa Ibanda - Mkolani Wilayani Nyamagana kwenye familia ya Mzee Frednand Zephania yenye wanafamilia 4 wanaosumbuliwa na maradhi ya kutetemeka pamoja na kupooza mwili na kisha kuwapatia msaada.

Amesema alipata mfadhaiko sana baada ya kuona taarifa hiyo kwenye vyombo vya habari na akaagiza wasaidizi wake kufuatilia tatizo ni nini lakini pia mahitaji ya kuweza kuwasaidia familia hiyo na ndipo amefika kuona namna gani watapata matibabu.

Mhe. Mtanda mara baada ya kupata taarifa kamili kutoka kwa wasaidiizi wake ndio akaamua kutafuta namna ya kupata bima za afya kwa wagonjwa zitakazowasaidia kupapatiwa matibabu bila ya kulipa kiasi chochote.

 “Bima hizi zina jumla ya gharama za shilingi milioni 2.1 ili kuwapunguzia mzigo wa gharama za matibabu ambapo mlikuwa mnalazimika kulipa fedha taslimu”. Amesema Mhe. Mtanda.

Sambamba na bima hizo, Mkuu wa Mkoa ameipatia familia hiyo mtaji wa biashara wa shilingi milioni tano (5) ili kusaidia mahitaji ya kila siku kama chakula na mahitaji mengine ya kila siku.

Katika hatua nyingine, Mhe Mtanda amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza kuwapatia familia hiyo kibanda cha kufanya biashara katika soko jipya la mjini kati ili mwanafamilia mmoja ambaye hajaathirika na changamoto hiyo aweze kufanya biashara na kumudu kuhudumia familia hiyo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wadau mbalimbali watakaoguswa na changamoto iliyoikumba familia hiyo kusaidia kuongeza mtaji kwa wanafamilia hao ili waweze kupata mtaji mkubwa zaidi huku akimtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba kuwapa kipaumbele wakati wote watapohitaji huduma za dharula wapate usafiri mara moja.

Vilevile, Mkuu wa Mkoa ameitaka jamii kuwapa moyo na kuendelea kuisaidia familia hiyo ili waweze kupata faraja kwa changamoto wanayopitia.

Mke wa Mzee Zephania Bi. Bahati Makalle amebainisha kuwa katika nyakati tofauti Mumewe na watoto wake watatu wamepatwa na ugonjwa huo wa kutetemeka na kupooza mwili, aidha alifanya jitihada za kuwapeleka kwenye uchunguzi na kuonesha wana shida ya misuli.

Katika kumudu maisha binti wa mwisho aitwaye Basilisa Zephania alikua anafanya biashara lakini aliifunga kutokana na kuhitajika kumsaidia mama yake kuwauguza wanafamilia hao ambao ni Samson zephania, Judith zephania, Nathan Zephania pamoja baba yao mzee Zephania.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema waliunda timu ya wataalamu kuchunguza chanzo cha tatizo hilo ambalo kwa awali wamebaini matatizo ya misuli na kwamba wanaendelea kufuatilia ili kubaini chanzo hasa ni nini.

Sambamba na hilo Dkt. Lebba pia  amewatoa hofu majirani wanaoishi kwenye mtaa huo kuchangamana na familia hiyo kwani uchunguzi wa kitaalamu unaonesha maradhi yanayowasumbua siyo ya kuambukiza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.