• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA Yatoa elimu kwa Wadau wa Huduma za Mawasiliano

Posted on: April 4th, 2019

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania  imefanya Mkutano na wadau  wa huduma za mawasiliano  Mkoa wa Mwanza  ikiwa na lengo la kukumbushana taswira ya Sheria ya Makosa ya Mitandaoni ya mwaka 2015,Matumizi bora ya mitandao ya kijamii,changamoto za watumiaji wa mawasiliano na kuelimisha Umma na utatuzi wa malalamiko hayo.

Akiongea katika kikao hicho Mkuu wa Kanda ya Ziwa Mamlaka ya Mawasiliano Mhandisi Fransis Mihayo amesema kutokana na ukuaji wa tekinolojia kumekuwa na uelewa mdogo wa watumiaji wa mitandao hivyo kifanya makosa ya kimitandao kuongezeka kila siku.

" Mamlaka inayo orodha ya watoa huduma mitandaoni wanaoendelea kurusha maudhui kwa kuvizia, inawataadharisha kuacha kuvunja sheria, bali wafuate taratibu za usajili,"alisema Mhandisi Mihayo.

Aidha amewaomba viongozi wa dini wakati wakiendelea kutujenga na kutuimarisha kiroho, watukumbushe pia uwepo wa changamoto ya matapeli mitandaoni na kamwe kila mtu hapaswi kutoa ushirikiano wa aina yoyote kwa kujibu ujumbe mfupi na kuendelea na mazungumzo na matapeli kupitia simu.

Naye Kamishna Msaidizi wa polisi Muliro J.MULIRO amesema maendeleo makubwa  ya kitekinolojia yameleta ongezeko kubwa la huduma mbalimbali mitandaoni, na kuleta msukumo mkubwa wa ukuaji katika Sekta ya mawasiliano.

"Mwaka 2000 kulikuwa na laini za simu 284,109 idadi hii imeongezeka hadi laini milioni 43 kwa sasa wakati huduma za intaneti wameongezeka  kutoka milioni 3 na laki tano kwa miaka 5 iliyopita hadi milioni 17 hivi leo," alisema Kamishna Muliro.

Kwa upande wao watoa huduma kutoka Vodacom wakiwakilishwa Mkuu wa Kanda ya Ziwa Victoria, Ayubu Kalutya  amesema wao hufanya kazi hadi jumamoai hivyo wangependa hata Jeshi la polisi lingefanya hivyo hasa wanaohuaika na taarifa ya upotevu 'loss report' kwani wateja huchukua muda mrefu kupata taarifa hii, pia huwachelewesha kurudisha line zao.

"Kuwe na udhibiti wa simu ili makampuni yanayotoa huduma za simu yaweze kuendesha huduma kuwezs kuwa na mawasiliano mazuri na wateja wao,"alisema Kalutya.

Aidha Mkuu Msaidizi wa Kitengo cha uhalifu wa kimtandao kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, ASP Joshua Mwangasa amesema, kuna changamoto kubwa ya kutoa taarifa za uongo hivyo jeshi la polisi linakabiliana na kila mvunjifu wa kosa hilo, hata hivyo ushirikiano mkubwa kati ya Jeshi la polisi na wananchi inasaidia kuleta amani.

"Ili kuepuka kufanya makosa ya mtandao  ni vema kufuata sheria,kuwa na hofu ya mungu, kuepuka kutuma taarifa udiyo na uhakika nayo na kuhakikisha kila mtu anatoa taarifa kwa jeshi la polisi pale ualifu unapotokea,"alisema ASP Mwangasa.

Aidha, ushirikiano unatakiwa ili kuleta amani kwani baadhi ya mitandao ya kijamii ipo nje ya nchi hivyo Mamlaka ya Mawasiliano haina mamlaka nayo.

Hata hivyo amesisitiza kuwa uvunjifu wote wa sheria uripotiwe polisi ili wahalifu wakabiliwe na sheria ifuate mkondo wake, pia ulinzi uanzie kwa mtu mwenyewe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.