• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TRA MWANZA WAANDAA FUTARI MAALUMU KUWASHUKURU WALIPA KODI KWA HIARI

Posted on: March 29th, 2025

TRA MWANZA WAANDAA FUTARI MAALUMU KUWASHUKURU WALIPA KODI KWA HIARI


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mwanza wameandaa futari maalumu kwa lengo la kuwapongeza Wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwa kulipa kodi kwa hiari ambapo mpaka kufikia sasa tayari Mamlaka wamefikia lengo kwa kukusanya mapato kwa 104%.

Akizungumza katika futari hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi amesema ulipaji wa kodi ndio msingi wa maendeleo ya Taifa, na kodi ndio uti wa mgongo wa miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa na inayopangwa kutekelezwa na serikali.

Aidha, amewapongeza kwa kufikia lengo la makusanyo ya asilimia 104 na kuwataka kuendelea kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa hiari, wananchi waelimishwe vizuri ili walipe kodi bila kushurutishwa na mtu yoyote kwa kuwa hayo ndio maelekezo na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mwanza Bw. Faustine Mdessa amesema walianza shughuli hiyo mapema jana ambapo walitoa msaada katika vituo viwili vya watoto yatima na leo wameamua kukutana na makundi mbalimbali ya wawakilishi wa wananchi kwa lengo la kuwashukuru na kurudisha shukrani kwa Wananchi.

“Niwaombe nyie ambao mmeshiriki sadaka hii maalumu muwe mabalozi wazuri wa ulipaji kodi mkawaambie wenzetu huko wawe wazalendo kwa kulipa kodi kwa hiari”.

Sheikh Wa Mkoa wa Mwanza Alhajj Hassan Kabeke naye amewapongeza Mamlaka hiyo kwa kufanya jambo jema la kuwakumbuka Yatima na wale wenye uhitaji, Aidha amesema katika mjumuiko huo kuna watu wa dini mbalimbali hiyo ikiwa ni ishara ya kwamba sisi Watanzania ni wamoja na hatuna budi kuendeleza mahusiano hayo mema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.