• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Uhifadhi wa Misitu wahimizwa Mwanza

Posted on: January 30th, 2022

Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii Mhe. Mary Masanja ametoa rai kwa viongozi wa Kanda ya Ziwa kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto za uhifadhi wa mazingira hususan katika mkoa wa Mwanza na Simiyu, lengo likiwa ni kuboresha maisha ya kila kiumbe ya sasa na siku za usoni.

Rai hiyo imetolewa leo mara baada ya kupokea taarifa ya Hali ya Uhifadhi  mkoani Mwanza ambapo Waziri alizitaka jamii za wakulima na wafugaji zinazoishi maeneo ya Hifadhi za Misitu ziishi kwa amani na kuhifadhi mazingira kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo.

Mhe. Masanja anasema miongoni mwa changamoto zinazowakabili wananchi wa vijiji vinavyouzunguka msitu nchini ni elimu juu ya uhifadhi na athari zake, namna wanavyoweza kutumia hifadhi za misitu kutokomeza umaskini pamoja na kutokuwepo na matumizi bora ya ardhi.

Kufuatia hali hiyo, Waziri ametoa rai kwa uongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania – TFS, viongozi wa Wilaya na Vijiji kushirikiana pamoja kuelimisha wananchi wanaozungumza hifadhi za misitu huku Wakala ukitakiwa kutafuta miradi kupitia programu za kurudisha kwa jamii (CSR) kusaidia jamii kando mwa misitu.

“Ninafahamu kuwa kuna Kamati ya Mawaziri nane iliyoundwa kushughulikia migogoro ya mipaka katika hifadhi yza misitu, lakini wakati tukishubiri kamati hiyo kutoa mapendekezo yake, tuanze sasa kutoa elimu na kuwafanyia vitu vingi vya CSR ikiwemo kuwapelekea miradi ya Ufugaji Nyuki pamoja na Kilimo na Ufugaji bora ili watuelewe, na wajue tunapohimiza uhifadhi tuna lengo zuri,” anasema Mhe. Masanja.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel anasema misitu iliyopo Kanda ya Ziwa haina hali nzuri na kuwataka viongozi kuchukua hatua za kuhimiza uhifadhi.


“Msitu yetu tumeiona kwenye ramani kubwa ya Kanda ya Ziwa hapa, niwaombe viongozi tuwe na moyo wa kihifadhi, kanda hii kuna maeneo yalikuwa na mvua mara mbili kwa mwaka na sasa mvua ni zakubahatisha huku maeneo mengine yakikumbwa na ukame, hakuna muujiza ni uhifadhi. Kuna maeneo yalikuwa na mito mikubwa sasa imekauka na ng’ombe wamekufa, tuna haja kubwa yakuwekeza kwenye mabadiriko ya tabia nchi,” anasema Mhe.  Mkuu wa Mkoa.

Anaongeza kwa kusema kuwa “viongozi wote kwa pamoja tuwe na wimbo mmoja, waheshimiwa wabunge, viongozi wa Serikali Kuu, taasisi za umma na binafsi tushirikiane sote kwa pamoja tuhifadhi misitu yetu kwa faida ya kizazi kijacho ambacho tusipofanya maamuzi magumu leo hii hakitakuwa na furaha, tusiwe wabinafsi.”

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe.  Salum Kali, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria na wabunge wawakilishi wa wananchi wanaoishi kando mwa hifadhi za misitu walisema, uhifadhi nchini una faida kubwa, muhimu ni kuwepo na programu ya kutoa mafuzo ya uhifadhi sambamba na kuanzisha miradi yenye manufaa katika uhifadhi wa misitu na kuleta manufaa kwa wananchi.



Awali Kamishna wa Uhifadhi – TFS Prof. Dos Santos Silayo alisema Wakala uko tayari kushirikiana na viongozi wa Kanda ya Ziwa katika kuhakikisha kuhakikisha uhifadhi unafanikiwa.

Aidha alisisitiza  kuwa licha ya changamoto mbalimbali za uhifadhi nchini, Wakala utaendelea kuhakikisha kunakuwepo na usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu na nyuki ili kuchangia kikamilifu mahitaji ya kijamii, kiuchumi, kiikolojia na kiutamaduni kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.