• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vifaa Tiba vyakabidhiwa kuboresha huduma ya Afya

Posted on: June 6th, 2018


Ili Kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wanawake, wajawazito watoto wachanga na watoto chini ya mwaka mmoja kwa Mkoa wa Mwanza, vifaa tiba vyenye thamani zaidi ya million mia moja vyakabidhiwa.

Haya yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa tiba hivyo kutoka mradi wa afya ya mama na mtoto (IMPACT PROJECT) wilayani Ukerewe.

Alisema lengo kuu la serikali ni kushirikiana na mradi huo ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na watoto wachanga mkoani Mwanza.

"Leo nimekabidhi vifaa hivi vifaa tiba vilivyonunuliwa na mradi wa IMPACT, kwa ufadhili wa Serikali ya watu wa Canada (GAC) ambazo ni mashine za kutakasia vifaa 45, mashine za kupima wingi wa Damu 80, mashine za kupimia Pressure 80 + 80,Mashine za kupimia uzito za watu wazima105, mashine za kupimia uzito watoto wachanga 80, Seti za kuzalishia kwa njia ya kawaida 80 na drip standa vyote vitumike ipasavyo ili kutimiza malengo " alisema Mongella.

Naye Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Thomas Rutachunzibwa alisema takwimu za afya ya uzazi Mkoa wa Mwanza (2017) zinaonyesha kuwa vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga bado ni vingi ambapo kwa mwaka 2017 vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi vilikuwa 195 na asilimia 92 ya vifo hivyo vilitokea katika vituo vya kutolea huduma za afya, na vifo vya watoto wachanga katika umri wa mimba baada ya kuzaliwa vilikuwa 1452 na vifo vya chini ya mwaka mmoja vilikuwa 684.

Aliongeza kuwa vyanzo vya vifo hivyo kwa asilimia fulani vilitokana na uhaba wa vifaa tiba kwa ajili ya kusaidia huduma kwa Mama wajawazito na watoto wachanga.

Pamoja na jitihada hizo , Mkoa huo bado unakabiliwa na Changamoto kubwa ambazo ni pamoja na wanawake wajawazito kuchelewa kuanza kliniki, mila na Desturi potofu, mimba za mara kwa mara za mpishano mfupi kati ya mtoto na mtoto idadi kubwa ya akina mama kujifungulia nyumbani, elimu duni juu ya masuala ya afya changamoto katika mfumo wa rufaa haswa kwa maeneno yenye visiwa.

"Kweli uelewa duni wa dalili za hatari kwa mama mjamzito na mtoto Mchanga, ushiriki duni wa wanaume katika masuala ya afya ya uazi, uelewa duni juu ya lishe na ulaji unaofafaa kwa akina mama wakati wa ujauzito na wakati wa kunyonyesha na watoto kutonyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi 6 ya mwanzo, yote haya yanachangia hali duni ya afya ya Mama na mtoto na jamii kwa ujumla" alisema Rutachunzibwa.

Kwa upande wake Meneja mradi wa IMPACT Edna Selestine alisema kupitia utekelezaji wa mradi huo Shirika la Aga khan Development Network lina mikakati ya kupunguza vifo kwa kuboresha upatikanaji wa huduma na kuongeza matumizi ya huduma bora za afya kwa wanawake, wajaawazito, watoto wachanga na watoto chini ya mwaka mmoja.

Alisema ili kufanikisha malengo hayo, mradi huo umejikita katika Kutoa mafunzo maalum kwa watoa huduma za afya ili kuwajengea uwezo wa kutoa huduma stahiki kwa wakati muafaka, Kujenga majengo yanayolenga huduma za wajawazito na watoto wachanga katika vituo 24 vya kutolea huduma ndani ya Mkoa wa Mwanza na kuwezesha upatikanaji wa vifaa tiba vya kutolea huduma na kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

"Mradi huu utawezesha mafunzo mbalimbali ngazi ya jamii ikiwa ni pamoja na vipindi vya Redio , Televisheni, vikundi mbalimbali ili kufikisha jumbe zitakazowezesha mabadiliko ya tabia katika jamii ili mwisho wa mradi huu baadhi ya changamoto kama si zote zinazochangia vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga vitapungua au kuisha kabisa",alisema Selestine.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.