• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WACHEZAJI WA PAMBA JIJI FC WAOGA NOTI, RC MTANDA AWAPA SOMO WAAMUZI

Posted on: February 10th, 2025

WACHEZAJI WA PAMBA JIJI FC WAOGA NOTI, RC MTANDA AWAPA SOMO WAAMUZI


Wachezaji wa timu ya soka ya Pamba Jiji FC wameoga noti shilingi milioni 15 na kuahidiwa nyongeza nyingine kama hiyo ndani ya siku chache kama muendelezo wa motisha huku Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda akiwakumbusha waamuzi kuzingatia sheria 17 za mchezo wa soka.

Katika hafla fupi ya kuwakabidhi fedha hizo iliyofanyika leo Februari 10,2025 kwenye uwanja wa michezo wa shule ya Sekondari Lake, RC Mtanda amebainisha  kuwa soka ni mchezo wa burudani na amani lakini akitokea mwamuzi na tafsiri tofauti atasababisha jazba na vurugu.

"Rai yangu kwa waamuzi, sasa hivi ligi kuu ipo hatua ya lala salama waamuzi wadumishe amani michezoni kwa kuchezesha kwa haki dimbani, mashabiki wanapenda burudani na siyo vinginevyo”. amesisitiza Mhe. Mtanda ambaye pia ni mlezi wa timu ya Pamba Jiji.

Katika hafla hiyo Mkuu huyo wa Mkoa amefafanua kila ushindi kwa timu za uzito wa juu kama Simba, Yanga na Azam motisha itakuwa shilingi milioni 15 huku Ile walivyokubaliana na uongozi kwa timu nyingine ushindi motisha ni shs milioni 10.

"Nimeahidi kwa ushindi dhidi ya Azam tutawapa shs milioni 15 lakini kuna baadhi ya wadau wa soka wa Mkoa wetu wamefurahishwa na mwendo mzuri wa timu na kuniunga mkono kwa kunichangia fedha, sasa baada ya siku chache nitawakabidhi shs milioni 15 nyingine na kufanya jumla iwe milioni 30”. Mhe. Mtanda.

Mfungaji wa bao la ushindi mchezaji Deus Kaseke amekabidhiwa kitita cha sh. laki saba na nusu, mfungaji wa bao lililokataliwa Salehe Masoud ameondoka na kibunda cha laki mbili na nusu, mchezaji aliyetoa pasi iliyozaa bao la ushindi Yonta Camara amepata sh. laki moja pamoja na mlinda mlango Yona Amos amekabidhiwa laki moja kwa muendelezo wa kutoruhusu nyavu zake kutikiswa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewaomba wale wadau wenye nia njema na Pamba Jiji walete michango yao kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa au Mkurugenzi wa Jiji ili kuzidi kuwapa motisha wachezaji wa timu hiyo ambayo Jumamosi hii watawakaribisha Coastal Union kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

Pamba Jiji FC maarufu kama TP Lindanda Wana Kawekamo baada ya ushindi dhidi ya Azam FC imechumpa hadi nafasi ya 12 na mtaji wa pointing 18 kibindoni katika msimamo wa ligi kuu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.