• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAFUGAJI MWANZA WATAKIWA KUFUGA KISASA KUKIDHI MAHITAJI SOKO LA NYAMA KIMATAIFA

Posted on: September 2nd, 2024

WAFUGAJI MWANZA WATAKIWA KUFUGA KISASA KUKIDHI MAHITAJI SOKO LA NYAMA KIMATAIFA


Mkuu wa mkoa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wafugaji Mkoani humo kuachana na ufugaji wa kienyeji wa mazoea na kufuga kisasa mifugo yao ili wakidhi mahitaji ya soko la nyama kimataifa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Septemba 2.2024 alipotembelea kiwanda cha nyama cha Chobo Investment kilichopo wilayani Misungwi kujionea uzalishaji na uchakataji nyama unaofanywa na kiwanda hicho.

Amesema nchi yetu ina zaidi ya ng'ombe Milioni 40 na inashika nafasi ya pili kwa ufugaji ng'ombe ikitanguliwa na Ethiopia lakini ni asilimia 5 tu ya mifugo hiyo ndio wanafaa kwa uzalishaji nyama hiyo, hali inayopelekea pia kutokufanya vizuri katika uchangiaji wa pato la Taifa ambapo kwa sasa ufugaji unachangia kwa asilimia 7 tu.

Aidha, amempongeza mwekezaji huyo kwa kupanua kiwanda hicho kwa dola za kimarekani milioni 3 zaidi kutoka kwenye 10 za awali zilizolenga kuongeza uchakataji wa mazao ya nyama kutoka matumizi ya 47% hadi 100% na kwamba itasaidia pia kupatikana kwa bidhaa 153 zinazotokana na mfugo ng'ombe.

Naye, Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bw. John Chobo amesema kiwanda chao kina uwezo wa kuchinja ng'ombe 600 kwa saa 8 lakini kwa sasa wanachinja 200 tu huku wakipata mbuzi wachache kutokana na uzalishaji kuwa wa kiwango cha chini na usiokidhi mahitaji.

Amefafanua kuwa ili kufikia malengo ya kupata nyama ya kutosha wameanzisha shamba ambalo wanafuga kisasa, wananenepesha na kuandaa malisho bora kwa mifugo na akatumia wasaa huo kuwakaribisha wafugaji kwenda kujifunza ili wazalishe kisasa.

"Kiwanda chetu ni kikubwa na tumekiongezea nguvu hivyo tunatamani kupata ng'ombe wenye uzito mkubwa hadi wa Kilogram 700 kwani mahitaji ya nyama kwenye soko la ndani na nje ni makubwa sana lakini kunakua na uhaba kutokana na ng'ombe wa asili kuwa na uzito mdogo." Amesema Bwana Chobo.

Vilevile, ametoa wito kwa sekta ya kilimo kuchangia kwenye ukuaji wa nyama kwa kuzalisha vifungashio vitokanavyo na zao la pamba linalofanya vizuri nchini (Mutton Cloth) vinavyotumika kuhifadhi nyama kwenda nje ya nchi tofauti na hali ya sasa ambapo vinaagizwa kutoka Vietnam.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA

    May 13, 2025
  • RC MTANDA ASISITIZA UIMARISHWAJI WA UMOJA NA MSHIKAMANO

    May 12, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.