• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAHITIMU AFYA WAASWA KUTUMIA ELIMU KUCHOCHEA MABADILIKO YA JAMII

Posted on: December 21st, 2025

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewaasa wahitimu wa kutoka sekta ya afya kutumia elimu waliyoipata kuitumikia jamii si tu kwa utabibu bali kwa kuleta fikra chanya zenye kuleta mabadiliko ya kifikra na kuweza kulinda afya zao.

Dkt. Lebba amesema hayo kwenye mahafali ya kumi na mbili ya chuo cha afya Tandabui yaliyofanyika Desemba 21, 2025 wakati akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Amesema taifa linahitaji wataalamu wa kutosha haswa katika fani za afya ambao watashughulika na afya za wazalishaji ambao watalisaidia taifa kufikia uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda.

“Ili Tanzania iweze kuwa nchi ya uchumi wa kati inayoongozwa na viwanda ni lazima kuwa na wataalamu wa kutosha katika fani za Afya ambazo zitashughulika na kuimarisha Afya za wazalishaji katika uchumi wa kati Wataalamu hawa hupatikana pale inapotolewa elimu iliyo bora na walimu walio makini”. Amesema Dkt. Lebba.

Aidha, amesema serikali imejipanga kuendelea kuimarisha na kuboresha sekta ya afya na kuleta maendeleo endelevu hususani kwa Mkoa wa Mwanza ambapo jumla ya Shilingi Bilioni 63.2 zimetolea kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya afya.

“Kuna miradi mikubwa ya serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika katika kipindi cha awamu ya sita hapa mkoani Mwanza ambapo jumla ya Shilingi Bilioni 63.2 zimetolewa katika Sekta ya Afya kwa ajili ya kuboresha miundombinu na ununuzi wa dawa na vifaa tiba”. Amesema Dkt. Lebba.

Sambamba na hayo ameupongeza uongozi wa wa chuo cha afya Tandabui kwa kutoa elimu bora na kuzalisha wataalamu kupitia ufundishaji unaozingatia mitaala ya ya afya inayoendana na uhitaji wa soko la ajira.

“Nawapongeza Tandabui kwa juhudi zenu za kubuni na kuboresha ufundishaji wenu kwa kuzingatia mitaala ya afya ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira na kukabiliana na uhaba wa wataalamu nchini katika fani za afya”. Ameongeza Dkt. Lebba.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.