• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WATUMISHI RS MWANZA WAFANYA ZIARA UTALII WA NDANI HIFADHI YA SERENGETI

Posted on: February 14th, 2025

WATUMISHI RS MWANZA WAFANYA ZIARA UTALII WA NDANI HIFADHI YA SERENGETI


Watumishi zaidi ya 30 kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo Februari 14, 2025 wamefanya ziara ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SNP) kwa ajili ya kushuhudia vivutio mbalimbali vya utalii.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, kiongozi wa msafara huo Mkuu wa Seksheni ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi ndugu Kusirie Swai amesema ziara hiyo imelenga kutoa hamasa ya utalii wa ndani kwa watumishi wa Mkoa wa Mwanza.

Amesema sambamba na hilo ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutangaza na kukuza sekta ya utalii nchini kwa kutembelea vivutio mbalimbali.

Ndugu Swai amesisitiza kuwa ziara hiyo imewapa fursa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwemo wanyama wakubwa kama vile Simba, Tembo, Faru, Nyati na Chui wakiwa katika mazingira ya asili yaliyohifadhiwa vizuri.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba akiwa ni miongoni mwa watumishi walioshiriki ziara hiyo ameushukuru uongozi wa Mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Said Mtanda na Katibu Tawala Mkoa Bw. Balandya Elikana kwa juhudi kubwa wanazofanya kwa watumishi hao ambapo wameitaja ziara hiyo kuwa itakwenda kuongeza tija na hamasa katika utendaji wa majukumu yao kutokana na mapumziko mujarabu.

"Ziara hii ya kitalii itasaidia kuhamasisha watumishi wengi zaidi kutembelea hifadhi wakiwa na familia zao wakati mwingine kwa kuwa wameshaona umuhimu wa kufanya hivyo kiafya kwani inapunguza hata msongo wa mawazo”. Amesema ndugu Paulo Zahoro, Afisa Habari wa Mkoa.

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni mbuga kubwa ya kitaifa ambayo ina urefu wa zaidi ya kilomita za mraba 14,763 Ipo mashariki mwa Mkoa wa Mara na kaskazini mashariki mwa Mkoa wa Simiyu na ina zaidi ya hekta milioni 1.5 Hifadhi hiyo ilianzishwa mnamo 1940.


Aidha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni urithi wa Dunia iliyojaa wanyamapori zaidi ya wanyama milioni 2, simba 4000, chui 1000, duma 550 na aina 500 za ndege wanaishi katika eneo linalokaribia kilomita za mraba 15,000 kwa ukubwa.


Watumishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wapo kwenye mpango thabiti wa kupumzika kwa kufanya utalii katika hifadhi mbalimbali nchini pamoja ni kuangalia utekelezaji wa miradi ya Kimkakati ambapo kesho februari 14, 2025 wanatarajia kutembelea Mamlaka ya Ngorongoro.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.