• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI BASHUNGWA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUIMARISHA USAFIRI VISIWANI

Posted on: October 11th, 2023

WAZIRI BASHUNGWA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUIMARISHA USAFIRI VISIWANI


Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga Fedha nyingi kukarabati na kujenga vivuko vipya katika kuimarisha Usafiri kwa wananchi wanaoishi maeneo ya Visiwa kwenye Mikoa ya Kanda ya ziwa.

Ametoa pongezi hizo leo Oktoba 11, 2023 wakati wa ziara yake Mkoani Mwanza alipofika kwenye Karakana na Songoro Marine wilayani Ilemela kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Vivuko vipya Vitano vilivyogharimu zaidi ya Bilioni 20 na Ukarabati wa Vingine kikiwemo Kivuko cha MV Mara kilichogharimu zaidi ya Milioni 300.


Aidha, amewaagiza Kampuni ya Songoro Marine kuhakikisha wanakamilisha asilimia moja iliyobaki kwenye Ukarabati wa Kivuko cha MV Mara kwa mujibu wa Mkataba kufikia Oktoba 15, 2023 ili kikahudumie wananchi kwenye visiwa vya Wilaya ya Musoma ambao wanakosubiri.

"Nimefurahi kuona Songoro Marine mnajitangaza kwa kazi nzuri kimataifa, ongezeni nguvu mfanye kazi usiku na mchana ili kufikia Oktoba 15, 2023 mkamilishe ukarabati na niwatake TASAC kuja kukikagua kwa haraka ili kivuko hichi (MV MARA) kikawaondolee adha ya Usafiri wananchi wa Mara." Waziri Bashungwa.

Vilevile, Waziri Bashungwa ameagiza ukamilishaji wa Vivuko vya Rugezi- Kisorya (70%), Ijinga- Kihangara (67%), Bwiro- Bukondo (70%), Nyakalilo- Kome (55.5%), Butagu -Mbalika (30%), MV Nyerere na MV Kilombero ili vikawahudumie wananchi na kutimiza adhma ya Rais Samia ya kuboresha huduma za Usafiri wa Majini.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuboresha huduma za Usafiri kwa kuhakikisha wananchi wanapata vivuko ambavyo ni bora na salama viwapo majini na amempongeza Mkandarasi Mzawa Songoro Marine kwa utekelezaji wa miradi kwa uzalendo.

"Hapo zamani kwenye maeneo ya ziwa kulikua na ajali za mara kwa mara kutokana na kutumia Mitumbwi ambayo sio salama, Mhe. Rais amedhamia kufuta kabisa adha hizo na kwa upendo mkubwa tunaona amekua akileta mabilioni ya fedha kwa ajili ya kukarabati na kujenga vivuko katika maeneo mbalimbali". Amesema Mkuu wa Mkoa.


Katika wakati mwingine Waziri Bashungwa amehudhuria Mkutano wa Bodi ya Usajiri wa Makandarasi na amewataka wakandarasi wa ndani kuheshimu taaluma yao, kuwa wabunifu na kuhakikisha wanatekeleza miradi katika hali ya ubora ili kulinda fedha nyingi zinazotolewa na Serikali na kujiweka katika nafasi nzuri ya kuaminiwa.

Akihitimisha ziara yake Mkoani Mwanza, Waziri Bashungwa amekagua ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi lenye urefu wa Kilomita 3.2 linalojengwa kwa zaidi ya Bilioni 700 na amemuagiza Mkuu wa Mkoa kumsimamia Mkandarasi anayejenga daraja hilo ili akamilishe kwa wakati kwani serikali inafanya malipo kila wakati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.