• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI NDEJEMBI AUNDA KAMATI KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI MWANZA

Posted on: February 10th, 2025

WAZIRI NDEJEMBI AUNDA KAMATI KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI MWANZA


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amemuagiza Kamishna wa Ardhi nchini Bwana Mathew Mhonge kuunda kamati mara moja kwa ajili ya kushughulikia mgogoro wa ardhi kwa kiwanja namba 01, Kitalu R kilichopo mtaa wa barabara ya Nyerere .

Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo leo Februari 10, 2025 akiwa kiwanjani hapo jijini Mwanza alipofanya ziara mahususi kwa ajili ya kushuhudia na kusikiliza pande mbili za malalamiko baina na mmiliki Z.E.K Ladhan Ltd na Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Waziri huyo ameagiza hadi kufikia ijumaa ya wiki hii (februari 14) kamati hiyo iwe tayari imepatikana ikihusisha wajumbe kutoka Wizara yake na Mkoa wa Mwanza aidha ifanye kazi ya kupitia nyaraka kwa siku saba kuanzia februari 17, 2025 na itoe mapendekezo ya nani mmiliki halali na nini kifanyike.

Sambamba na hilo ametoa wito kwa jamii kuendelea kufuata sheria wakati wanapotaka kumiliki ardhi ili kujiepusha na migogoro na kwa upande wa watumishi wa serikali (Sekta ya Ardhi) amewasihi kuendelea kufanya kazi kwa kufuata maadili ya utumishi wao kwa mujibu wa kanuni na sheria.

Akijibu hoja ya mwananchi mmoja aliyetaka kufahamu hatma ya wananchi waliovamia eneo la Mamlaka ya Viwanja vya ndege katika Manispaa ya Ilemela na kuzuiwa kuviendeleza, Mhe. Ndejembi amesema serikali inashughulikia suala hilo na siku za usoni itaketi nao kuzungumza na kumaliza mgogoro huo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Waziri wa Ardhi kwa utendaji wake unaolenga kumaliza migogoro ya ardhi nchini hususani mkoani humo na amemuahidi kushiriki vema kwenye uundaji wa kamati hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.