• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wilaya ya Magu yavuka lengo ujenzi wa vyumba vya madarasa

Posted on: January 5th, 2023

*Wilaya ya Magu yavuka lengo kwa Ujenzi wa vyumba vya Madarasa*


Bilioni 3.26 zajenga Madarasa 163 wilayani Magu kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 na kupelekea wilaya hiyo kuwa na ziada ya vyumba saba vya Madarasa ambavyo vitatumiwa na vidato vingine kutokana na mahitaji kuwa ni vyumba 271 kutokana na uwepo wa vyumba 115 hivyo kupelekea kuwa na vyumba 278.

Hayo yamebainishwa leo (Januari 04, 2023) wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika kwenye shule ya Sekondari Magu iliyojengewa vyumba 12 vya madarasa kati ya shule 28 zilizopata mradi huo ambapo kwa wilaya nzima jumla ya wanafunzi

10823 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.

Akizungumza na wananchi kwenye uzinduzi wa Madarasa hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ametoa pongezi kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upendo wake kwa wanafunzi kwa kuamua kuwaboreshea mazingira ya Elimu.

"Kwa mikoa yote nchini sisi Mwanza ndio tumeongoza kwa kupewa Madarasa 983 kupitia mradi huu, nawasihi wananchi tusiache kumuombea dua Rais wetu mpendwa kwa Mwenyezi Mungu ili amjaalie afya njema aendelee kuwahudumia wananchi wake." Malima.

Amesema, Serikali inatarajia ongezeko kubwa la wanafunzi kutokana na jamii kuzidi kuzaliana na kwamba imejipanga kuendelea kuboresha Miundombinu si tu ya wanafunzi bali na walimu na ametoa rai kwa wanafunzi kutunza madarasa na samani na kusoma kwa bidii ili ufaulu upande.

"Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwani kila shule wilayani kwetu imefikiwa na mradi huu kwa kupata idadi tofauti ya vyumba vya Madarasa lakini tumepata pia shule mbili mpya kabisa na ilipofika tarehe 24, Disemba 2022 tulikua tumeshakamilisha ujenzi wa madarasa haya." Amesema Mkuu wa wilaya ya Magu, Mhe. Salum Kalli.

Afisa Elimu Sekondari wa wilaya hiyo Bi. Beatrice Balige amesema pamoja na ukamilishaji wa madarasa hayo jumla ya seti za viti na meza 6520 vipya vimetengenezwa na kufikia lengo la uboreshaji wa Elimu kwa kuwafanya watoto waketi kwenye Madarasa yanayochagiza ufundishaji na kujifunza kwa ufanisi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.