• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA BILIONI 40 KUJENGA MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI MWANZA, GEITA

Posted on: August 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya Tshs. Bilioni 40 kwa ajili ya kujenga na kukarabati miradi tisa ya umwagiliaji inayotarajia kuwanufaisha zaidi ya wakulima elfu 40 Mwanza na Geita .


Amebainisha hayo leo agosti 08, 2025 alipokua akihutubia maelfu ya wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali katika kilele cha maadhimisho ya nane nane kanda ya ziwa magharibi yanayofanyika katika viwanja vya Nyamhongolo wilayani Ilemela.


Kadhalika ameeleza kuwa kwa kipindi cha 2020/25 serikali imetoa mbolea ya ruzuku ya Bilioni 6.4, Bilioni 4.7 kwa ajili ya ufugaji wa kisasa kwa vizimba ambapo zaidi ya vikundi 200 vimenufaika na Bilioni 263 zimetolewa kwa ajili ya chanjo za kuku na ng'ombe ndani ya mikoa hiyo.


Aidha, ameziagiza halmashauri kuendeleza viwanja hivyo kwa kuvijengea miundombinu ya kudumu na ya kisasa ili viwe na mazingira bora zaidi ya kuwahudumia wananchi katika kutoa elimu ya mashamba darasa kwa muda mrefu.


Akitoa taarifa ya maonesho hayo, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Bw. Peter Kasele amesema wadau wameongezeka kutoka 1110 (2024) hadi 1234 (2025) ikiwa ni ishara ya wananchi kuhamasika kutaka kujua matumizi ya teknolojia katika kuongeza uzalishaji.


Aidha, ametaja changamoto ya kukosekana kwa miundombinu ya kudumu kwa ajili ya mashamba darasa na kusababisha gharama za mara kwa mara kwa kuweka miundombinu ya muda mfupi kila mwaka mathalani vipando, majosho, wajasiriamali, mabwawa ya uvuvi wa kisasa na maeneo ya unenepeshaji wa mifugo.


Ndugu Wenceslaus Venant ambaye ni mkulima kutoka Kisesa wilayani Ilemela aliyekopeshwa trekta la kisasa kwa ajili ya kilimo na benki ya Azania kwa kushirikiana na Agricom ameishukuru serikali kwa kujenga mazingira rafiki kwa taasisi za kifedha na kuweza kutoa mikopo kwa wakulima pamoja na wafugaji.


Kilele cha maonesho hayo kimechagizwa na utoaji tuzo na zawadi ambapo Aqwa Eagle (Magu) wameongoza katika uvuvi wa samaki, Fresrick Katundala (Nyamagana) ufugaji Nyuki, Mkulima bora akiwa ni ndugu Bulimi Zakaria (Kwimba) na Shija Mashauri (Nyang'hwale) akiibuka kidedea kwenye ufugaji bora wa ng'ombe wa nyama

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BILIONI 40 KUJENGA MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI MWANZA, GEITA

    August 08, 2025
  • WANAHABARI, JESHI LA POLISI WAASWA KULINDA AMANI KIPINDI CHA UCHAGUZI

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.