• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

AFISA ELIMU MWANZA AWATAKA MAAFISA TAKWIMU KUHALALISHA UWEPO WAO

Posted on: August 15th, 2024

AFISA ELIMU MWANZA AWATAKA MAAFISA TAKWIMU KUHALALISHA UWEPO WAO


Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Mwl. Martine Nkwabi amewataka Maafisa Takwimu wa Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kuhalalisha uwepo wao kwa kufanya kazi kwa bidii na kuboresha utendaji kazi wao ili kuifanya kazi ya kitengo hicho kuonekana.

Mwalimu Nkwambi ametoa wito huo leo Agosti 15, 2024 wakati alipokuwa akifungua kikao cha Maafisa Vifaa na Takwimu Msingi na Sekondari kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mwl. Nkwabi amesema kwa kipindi cha hapo nyuma kumekuwa na vitengo mbalimbali ndani ya Idara ya Elimu lakini kutokana na kutofanya vizuri kwa vitengo hivyo vimefutwa hivyo amewataka Maafisa hao pia kubadilika na kuhalilisha uwepo wao.

"Sisi tunatakiwa kubadilisha utendaji kazi wetu, Katika miaka kama 20 hivi vitengo katika Idara ya Elimu zimekuwa zikibadilika badilika kwa sababu wale waliopewa majukimu hayo walishindwa kuhalalisha zile nafasi zilizokuwepo na mimi sitaki yawakute hayo". Amesema.

Takwimu za elimu ni nyingi sana ndio maana mkawekwa nyinyi kuna takwimu za vitabu, kuna idadi ya Wanafunzi wenye ulemavu, Afisa Michezo anahitaji takwimu za Wanafunzi wanaoweza kucheza michezo mbalimbali, mkifanya vizuri katika uratibu wa sekta yenu hamtoamini mtakuwa mnatafutwa sana huko kwenye Halmashauri zenu kwa sababu kila mtu atahitaji kupata takwimu sahihi kutoka kwenu. Ameongeza Afisa Elimu.

Sambamba na hayo Afisa Elimu huyo amewataka Maafisa hao kuhuisha takwimu zao mara kwa mara kwa sababu mambo hubadilika, takwimu za mwaka jana sio za mwaka huu mambo mengi hapa kati yanatokea ikiwemo uhamisho wa Waalimu na Wanafunzi, Walimu wanaokwenda kusoma.

Aidha Afisa Elimu huyo amewataka Maafisa hao kufanya kazi kwa ushirikiano na Maafisa wengine kutoka Idara za Elimu kwani wote ni watumishi wa elimu na ikitokea unahitajika msaada wowote katika Idara basi mtu yoyote aweze kufanya shughuli hiyo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti