SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
Wilaya ya Ukerewe ni miongoni mwa wilaya zilizonufaika na ajira mpya kufuatia ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa kampeni za mwaka 2025.

Ndani ya siku 100 za uongozi wake, wilaya hiyo imepata ajira 127 katika sekta ya afya na ajira 25 katika sekta ya elimu, jumla ya watumishi 152.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amewataka watumishi waliopangiwa vituo wilayani humo kuripoti kazini mara moja bila visingizio.

Amesisitiza kuwa hakuna sababu ya kuhamisha watumishi kwani Ukerewe ni sehemu salama na halali ya ardhi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Mkoa wa Mwanza pekee umepata ajira 1,236. Ukerewe ni miongoni mwa wilaya zilizopewa watumishi wengi wa sekta ya afya,” amesema Mkuu wa Mkoa