• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BITEKO AWATAKA WAANDISHI WAENDESHA OFISI KUJIENDELEZA KITAALUMA

Posted on: May 23rd, 2024

BITEKO AWATAKA WAANDISHI WAENDESHA OFISI KUJIENDELEZA KITAALUMA


*Amewataka Waajiri kujali maslahi ya kada ya Waandishi Waendesha Ofisi*


*RC Mtanda amemshukuru Rais Samia kwa Utekelezaji wa miradi Mikubwa Mwanza*


*Abainisha pia utoshelevu wa Umeme kwa wananchi wa Mkoa huo*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Waandishi Waendesha Ofisi kujiendeleza kitaaluma ili kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia hususani kidigiti kwani ndiko kwenye muelekeo wa dunia ya sasa.

Amesema hayo leo 23 Mei, 2024 wakati akifungua rasmi Mkutano wa kumi na moja wa Kitaaluma wa Waendesha Ofisi unaofanyika kwa siku sita kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza chini ya Uratibu wa Chama cha Makatibu Mahsusi (TAPSEA).

Dkt. Biteko ametoa wito kwa waandishi waendesha ofisi hao kubadilisha utendaji kazi kwa kujali wananchi na kuhakikisha wanatatua changamoto zao kwa upendo na uamuzi bora wa utendaji kazi ili kuleta tija kwa Serikali yenye matarajio makubwa kwao.

Aidha, ameziagiza Wizara husika kuhakikisha wanakomesha kero na changamoto zinazowakabili waandishi waendesha ofisi hao kwa kuzingatia matakwa ya muundo mpya wa utendaji wa kada hiyo na kuhakikisha waajiri wanajali maslahi yao.

Mhe. George Simbachawene (MB), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora ametumia jukwaa hilo kuwataka kuwa mabalozi wazuri kwa waajiri wao kwa kuwa wabunifu na wenye utendaji kazi wa kuzingatia maadili zaidi na ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuboresha kada hiyo.

Hata hivyo, ameahidi kutoa waraka kwa taasisi zote kuboresha muundo wa waandishi waendesha ofisi kwa kuzingatia majukumu mapya yanayoenda sambamba na muundo mpya wa kada hiyo ulioanza mwezi Juni 2023 baada ya Mhe. Rais kuridhia maboresho ya kada hiyo ikiwa ni pamoja na ajira kuanza na ngazi ya stashahada.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaja miradi inayotekelezwa Mwanza kama  wa Umeme Vijijini wa REA wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 56 kabla ya ile ya Ujazilizi inayogharimu zaidi ya Bilioni 12 na amebainisha kuwa Mwanza inatumia Megawati 76 pekee za umeme pamoja na kuwepo kwa Megawati 153.

Vilevile, ameitaja miradi ya upanuzi na uboreshaji wa Uwanja wa Ndege, ujenzi wa Meli ya kisasa ya MV Mwanza, mradi wa maji Butimba, ujenzi wa vivuko vya kisasa na akabainisha kuwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha umahiri mkubwa kwenye kuongoza Taifa kwani miradi hiyo ipo kwenye hatua za mwisho za ukamilishaji.

Mwenyekiti wa TAPSEA Bi. Zuhura Songambele amesema chama hicho kipo imara huhakikisha kinakuza uwajibikaji, kusaidia wanachama kuendeleza taaluma yao pamoja na kuwakumbusha kutoa huduma bora kwa viongozi na wananchi kwa weledi.

Mkutano huo wa kumi na moja uliowakutanisha zaidi ya wanachama elfu tano unaendeshwa kwa juma zima chini ya Kauli Mbiu isemayo ; Mafanikio huanza na uamuzi bora wa Utendaji, tutumie muda vizuri kwa kufanya kazi na kuleta Tija.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti