• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BOTI YA KISASA KURAHISISHA UOKOZI NA MATIBABU UKANDA WA ZIWA- RC MTANDA

Posted on: July 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo julai 07, 2025 amekagua Meli ya Kisasa ya Uokozi na Matibabu iliyojengwa kwa gharama ya Tshs. Bilioni 4.5 chini ya mradi wa Kikanda wa Usafiri na Mawasiliano Ziwa Victoria unaojumuisha nchi ya Tanzania na Uganda.


Akizungumza wakati wa majaribio kutoka bandari ya Mwanza Kaskazini na kurudi Mkuu wa Mkoa ameishukuru serikali ya awamu wa sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona umuhimu wa kuwekeza kwenye eneo la ziwa victoria ili kuhakikisha wananchi wake wanakua salama wanaposafiri na kufanya shughuli za uvuvi.

“Tunashukuru Serikali ya awamu ya sita kwa utekelezaji wa mradi huu ambao unakaribia kukamilika”.



Na moja ya mambo yaliyo chini ya mradi huu ni pamoja na kuweka mawasiliano na kujenga kituo cha Kikanda cha kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji kilichopo Ilemela na ununuzi wa boti hii pamoja na boti mbili ndogo za utafutaji na uokoaji. Amesema Mhe. Mtanda.


Aidha, amesema boti hiyo ya kisasa italeta fursa kwa wagonjwa watakaopata dharula zozote ndani ya maji, boti hiyo itawafikia kwa haraka na kutoa Matibabu ya dharura kabla ya kufikishwa nchi kavu kwa ajili ya kupelekwa hospitali ya rufaa katika eneo husika.


Naye Afisa Mfawidhi Mkoa wa Mwanza kutoka Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Joseph Mkumbo amesema boti hiyo ya kisasa ina uwezo wa kutembea maili 18 kwa saa.

 Aidha, amebainisha kuwa imewasili mkoani Mwanza kutoka bandari ya Mtwara tarehe 23 Juni, 2025 na kwamba kwa ushirikiano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza walifanikisha kuishusha majini tarehe 05 Julai 2025 kwenye bandari ya Mwanza Kusini.


Ameongeza kuwa tayari TASAC wameifanyia majaribio majini na kuonesha mafanikio makubwa sana kwani imetumia muda wa saa 1 kwenda Ukerewe tofauti na meli zinazotumia masaa 3 hadi 4 na ameongeza kuwa mradi huo unahusisha pia ununuzi wa boti mbili zingine zenye vifaa.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti