• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BULABO IWE TAASISI ITAKAYOJISIMAMIA, YENYE WIGO WA KITAIFA NA KIMATAIFA: RC MTANDA

Posted on: May 10th, 2024

BULABO IWE TAASISI ITAKAYOJISIMAMIA, YENYE WIGO WA KITAIFA NA KIMATAIFA: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo ameendelea kukutana na makundi mbalimbali akianza mkutano wake na Machifu amesema mpango uliopo ni kuhakikisha Tamasha la utamaduni wa kabila la Wasukuma la Bulabo linakuwa ni Taasisi imara itakayojisimamia na kuwa na wigo wa mpana nchini na nje ya Tanzania.

Muendelezo wa mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe.Mtanda amebainisha kutokana na umuhimu wa tamasha hilo mwaka huu litakuwa na sura ya kikanda kwa kuunganisha mikoa ya Kanda ya ziwa na Tabora.

"Tayari tumefanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Prof. Adilaus Kilangi ametoa ushauri huo pia tamasha la mwaka huu  tumewaalika wenzetu kutoka huko Amerika ya Kusini pia na sisi tutakwenda huko kubadilishana uzoefu na kujifunza zaidi," Mkuu wa Mkoa.


Amesema tamasha hilo linapaswa kwenda pamoja na makongamano yatakayowahusisha wataalamu wa masuala ya utamaduni, vyakula vya asili na mavazi ili kila wakati wa maadhimisho hayo kuwepo na mabadiliko.

"Nawakikishia Machifu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imelipokea jambo hili na itatoka ushirikiano wa dhati kuhakikisha Bulabo ya mwaka huu inakuwa bora zaidi niwaombe sana Machifu tuendelee kuisaidia Jamii ili kujivunia mila na desturi zetu,"Mkuu wa Mkoa.

"Sherehe za mwaka huu zitafanyika Juni 22 badala ya mwanzoni mwa mwezi huo,hii ni kutokana na kuwashirikisha wenzetu kutoka Brazil ambao tarehe za mwanzoni hawataweza kufika,"Jackson Kadutu,Katibu wa Bulabo.

Katika mkutano uliofuata na Baraza la Wazee wa Mkoa wa Mwanza,Mkuu huyo wa Mkoa amesema Ofisi yake itaendelea kupokea ushauri wa masuala mbalimbali ya maendeleo na kuwakumbusha mamlaka husika kutoa kipaumbele kwa wazee katika suala la kupatiwa matibabu bure.

"Umoja huu una wanachama hai 38 na lengo letu ni kuishauri Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kufuatilia shughuli mbalimbali ikiwemo miradi inayoletwa na Serikali mkoani hapa,"Charles Masalakulangwa,Mwenyekiti Baraza la Wazee Mwanza.

Mkutano wake wa mwisho na wadau wa Sekta ya Utalii,Mkuu huyo wa Mkoa amepokea maoni namna ya kuiboresha sekta hiyo inayochangia 17% ya pato la Taifa na kutaka mikakati zaidi ifanyike kutokana na Serikali kuimarisha miundombinu ukiwemo upanuzi wa uwanja wa ndege.

"Niwape muda zaidi wa kukaa na kuona namna ya kuwashirikisha wadau wengine zaidi kabla ya sijaitisha  kikao kikubwa zaidi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti