• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

CUHAS BINGWA WA TAMSA CUP 2024/25, RMO MWANZA AWAPA KIKOMBE NA FEDHA TASLIMU

Posted on: March 1st, 2025

CUHAS BINGWA WA TAMSA CUP 2024/25, RMO MWANZA AWAPA KIKOMBE NA FEDHA TASLIMU


Katibu Tawala Msaidizi Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa amefunga rasmi michuano ya jumuiya ya wanafunzi wa udaktari kutoka chuo cha Bugando (CUHAS) na Mwanza University katika uwanja wa CCM Kirumba.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mtanange mkali wa fainali uliowapa ushindi timu ya Bugando waliowapa kichapo cha mabao saba kwa nunge vijana wa Mwanza University Dkt. Lebba amewapongeza washindi hao na amewakabidhi Kikombe pamoja na fedha taslimu kiasi cha Tshs. 750,000

Dkt. Lebba ametumia wasaa huo kuwapongeza wanafunzi hao kwa kuandaa michuano hiyo huku akibainisha kuwa michezo kama sehemu ya mazoezi inasaidia kuimarisha afya na kuondoa msongo wa mawazo na kuwafanya wawe timamu kiakili katika masomo darasani.

"Michezo ni sehemu ya mazoezi hivyo nawapongeza sana nyie binafsi kama Serikali ya wanafunzi kwa kuandaa michuano hii kwani itawaimarisha kiafya na kuwafanya muwe na utayari wa kupokea maarifa darasani." Dkt. Lebba.

Aidha, Mganga Mkuu amewapongeza wanafunzi hao kwa ubunifu hadi kufanikisha Kongamano la Kisayansi pamoja na kambi ya uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza matukio waliyoyafanya mwishoni mwa mwaka 2024 na kuleta tija kwa jamii na Taifa.

Michuano ya TAMSA CUP 2025 imefanyika katika Viwanja vya CCM Kirumba Wilayani Ilemela kwa kipindi cha mwezi mmoja huku ikizikutanisha timu sita kutoka kwenye vyuo hivyo viwili vya Afya na Sayansi chini ya kaulimbiu isemayo “Michezo kwa Afya Bora ya Akili”.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti