• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Daima tupo Tayari - Mongella

Posted on: March 23rd, 2020

Mwezi Novemba na Desemba 2019 pengine ni kati ya vipindi ambavyo mkoa wa Mwanza umeshuhudia na kupokea ugeni mkubwa Kitaifa na Kimataifa.

Ni kipindi hicho ndipo maadhimishi ya wiki ya siku ya Ukimwi yalipofanyika jijini Mwanza ikiwaleta pamoja viongozi wa Kitaifa na Kimataifa.

Kitaifa walikuwepo Mawaziri, Watendaji wakuu wa taasisi zinazohusika na mapambano dhidi ya Ukimwi, wasanii pamoja na wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wanaohusika na masuala ya Ukimwi (UNAIDS), wanawake (UN WOMEN na kazi (ILO).

Kilele cha maadhimisho hayo vilivyofanyika katika viwanja vya Rock city Mall vilishirikisha watu kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo vijana na wazee wake kwa waume.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ni kati ya viongozi wa Kitaifa waliofika Mwanza katika wiki ya siku ya Ukimwi kwa ajili ya kuhudhuria kongamano maalum lililoandaliwa na Kamati ya kupambana na Kifua Kikuu (TB).

Kongamano hilo lilijumuisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini na wastaafu wakiongozwa na Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda.

Orodha ya viongozi wa Kitaifa waliofika Mwanza kuanzia maadhimisho ya Ukimwi pia wamo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na wenye ulemavu) Jenista Mhagama na Katibu wa Baraza la Ulama Taifa Sheikh Hassan Said Chizenga.

Pia walikuwemo Makamu wa Pili wa Mwenyekiti wa Baraza la Makanisa Tanzania (CCT) Jacob Chimeledy na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge walio kwenye mapambano TB nje ya Bunge, Osca Mkasa.

Latola ngazi ya Kimataifa,

Mwanza pia imewapokea wawakilishi wakazi wa mashirika na taasisi za Umoja wa Mataifa walioongozwa na Mwakilishi mkazi wa UN AIDS, Dk Leo Zekeng.

Maadhimisho ya siku ya Ukimwi yameambatana na maadhimisho mengine ya siku 16 ya kupiga vita vitendo vya ukatili na unyanyasaji kujinsia dhidi ya wanawake na watoto ambapo hoja ya kuwepo pete tegesha za uchumba miongoni mwa wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu iliibuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Kivulini, Yassin Ally.

Taarifa za pete tegesha za uchumba na ndoa za kuwalaghai wanafunzi wa kike zimeigutusha Serikali ambayo kupitia Waziri Mhagama imetangaza kuitisha kikao cha wadau wote ifikapo Januari, 2020 kujadili na kutafutia ufumbuzi suala hilo.

Akihutubia kilele cha siku ya Ukimwi katika viwanja vya Rock city Mall kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Waziri Mhagama akautaarifu umma kuwa kikao hicho kitaandaliwa kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Wazira ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti