• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

Posted on: May 2nd, 2025

DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.


Serikali imetangaza kuwa daraja la JPM Kigongo-Busisi, linalounganisha wilaya za Sengerema na Misungwi mkoani Mwanza lipo tayari kuanza kutumika muda wowote kuanzia sasa baada ya kukamilika kwa zaidi ya asilimia 99 ya ujenzi wake.

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Gerson Msigwa wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa miradi ya kimkakati mkoani Mwanza ikiwemo ya vivuko na daraja hilo muhimu.

Msigwa amesema kukamilika kwa daraja hilo ni hatua kubwa ya maendeleo kwani linakwenda kumaliza changamoto ya usafiri kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya ziwa na hata wale wanaotoka nje ya nchi wanaovuka ziwa Victoria kuingia au kutoka mkoani Mwanza.

“Daraja hili linatarajiwa kuanza kutumika ndani ya mwezi Mei.Hii ni neema kwa Watanzania, hususan wa mikoa ya kanda hii, kwani litaimarisha biashara, usafiri na fursa nyingine za kiuchumi,” amesema Msigwa.

Aidha, Msigwa amesema serikali inaendelea kutekeleza miradi mingine ya kuboresha usafiri wa majini kwa kujenga vivuko vipya katika maeneo mbalimbali ya Ziwa Victoria ili kurahisisha huduma kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Msigwa ametembelea pia ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza ambao umefikia asilimia 96. Alisema kazi zilizobaki ni kufunga viti na vitanda, na meli hiyo itaanza kutoa huduma kwa wananchi muda si mrefu.

Ameeleza kuwa miradi hii yote ni sehemu ya dhamira ya serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha miundombinu ya usafiri na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa na Taifa kwa ujumla.

Katika ziara hiyo, Msigwa aliambatana na waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga, waliopata fursa ya kujionea maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo ya kimkakati.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti