• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Daraja la Simiyu lafungwa kupisha matengenezo

Posted on: March 6th, 2020


Daraja la mto Simuyu lililoko Wilayani Magu, barabara kuu ya Mwanza-Musoma limeharibika kutokana na uchakavu jambo lilipelekea vyuma kukatika lita fungwa kwa muda wa siku 10 ili kupisha utekelezwaji wa matengenezo makubwa .

Akiwasilisha taarifa ya ufungwaji wa daraja hilo Meneja  wa Tanroads Mkoa wa Mwanza Mhandisi Marwa M. Rubirya alisema watafunga barabara ya Mwanza- Musoma kuanzia Machi 8 hadi 18 mwaka huu ili kupisha matengenezo makubwa ya daraja hilo.

Mhandisi Rubirya ameongeza kuwa wameamua kufanya matengenezo ya haraka ili kujiepusha na hatari zitakazoweza kujitokeza kwa sababu kuchelewa kwa ujenzi huo yaweza kuwa hatarishi kwa watumiaji wa barabara hiyo .

Aliongeza kuwa barabara hiyo itafungwa ili kupisha matengenezo kuanzia saa tatu usiku hadi saa 11 asubuhi  pia aliomba ushirikiano wa Jeshi la polisi katika kutekeleza kazi hiyo.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa daraja hilo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella alisema kutokana na changamoto hiyo njia zitafugwa kwa muda uliopangwa  kwa siku  kumi ili kupisha matengenezo hayo.

Alisema Serikali inampango wa kujenga daraja jipya hivyo hatua zinazofanyika sasa  ni za muda mfupi, aliwataka wananchi kuwa wavumilivu waweze kuboreshewa njia itakayowanufaisha na kuendeleza ujenzi wa taifa.

" Hali halisi ilivyo na nyie mmeiona ninachowaomba muwe wavumilivu ujenzi ufanyike ili kuepusha madhara makubwa ya baadaye" alisema Mhe.Mongella.

Lusia Isack ni mmoja wa wakazi wa Magu akizungumzia adha hiyo alisema wanakuwa wa hofu kila wanapopita kwenye daraja hilo hasa wanapofika katikati hivyo wanaishukuru Serikali kwa kuliona hilo kwani wameweza kutatua changamoto hiyo kabla haijaleta maafa.

"Hili daraja ni bovu sana  ata ukiwa umebebwa kwenye baiskel ukifika katikati daraja linaanza kucheza sasa ukiwa kwenye gari unawaza sijui nitapita salama kwa sababu likidondoka tu sizani kama kuna mtu atakayepona kinachobaki ni kuomba Mungu wakitutengenezea watakuwa wametusaidia sana." alisema Isack.

Hata hivyo daraja hili lililojengwa mwaka 1962 limeanza kuonyesha nyufa baada ya vyuma vilivyokuwa vinalishikilia kukatika jambo hilo limejenga hofu kwa Serikali na watumiaji wa njia hiyo harakati za haraka zinafanyika ili kubadilisha vyuma hivyo .

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti