• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

DC MISUNGWI AAGIZWA KUMSIMAMIA MKANDARASI AKAMILISHE UJENZI WA SHULE YA AMAALI

Posted on: January 19th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Misungwi kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya hiyo kumtafuta na kumsimamia kikamilifu mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa Shule mpya ya Mtaala wa Ufundi (Amaali) ili ahakikishe anakamilisha mradi huo mara moja.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo katika kijiji cha Mungwe Wilayani Misungwi wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya shule hiyo inayogharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.6.

Akizungumza katika ukaguzi huo Mhe. Mtanda amesema Serikali haitakuwa na huruma kwa wakandarasi wanaochelewesha au kufanya kazi chini ya viwango vilivyokubaliwa.

“Hakuna huruma kwa watu wanaoichezea Serikali. Baadhi ya wakandarasi wananufaika na fedha za Serikali lakini wanajenga kwa uzembe, kuchelewesha kazi na kufanya ujenzi kwa mazoea yasiyokubalika,” amesisitiza.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto wa elimu ya awali kuanza masomo kwa wakati.

Ameeleza kuwa kati ya watoto 16,840 waliopaswa kuripoti shule, ni watoto 8,264 pekee ndio walioripoti. Vilevile, kati ya watoto 17,671 waliokusudiwa kuanza masomo katika ngazi nyingine, ni watoto 11,057 tu sawa na asilimia 62 ndio walioripoti wilayani humo.

Kutokana na hali hiyo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Misungwi kushirikiana na viongozi wa kata na vijiji kupita nyumba kwa nyumba kuwatafuta wanafunzi ambao bado hawajaripoti ili kuhakikisha wote wanaanza masomo bila kikwazo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti