• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

DC MKALIPA AVIPONGEZA VIKUNDI VYA JOGGING KWA KUANDAA TAMASHA LENYE HAMASA

Posted on: October 25th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Amir Mkalipa amevipongeza vikundi vya mbio za pole pole (Jogging) mkoani humo kwa kuandaa tamasha la kuwahamasisha wananchi kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

Amesema hayo akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza katikaTamasha la mbio za pole zenye lengo la kujenga afya na kupongeza maboresho katika sekta ya afya lililofanyika leo Oktoba 25, 2025 kwa kukimbia kuanzia viwanja vya Furahisha hadi hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure, kuchangia damu pamoja na kufanya usafi katika hospitali hiyo.

Ameongeza kwa kuishukuru serikali ya awamu ya Sita kwa kuboresha sekta afya mkoani humo kwa kuongeza ajira na kupunguza uhaba wa watumishi, kuleta vifaa tiba, madawa pamoja na kuboresha huduma za kibingwa katika hospitali ya Mkoa ya rufaa Sekou-Toure na hospitali ya kanda Bugando.

“Zaidi ya watumishi 600 wameongezeka sekta ya Afya mkoani Mwanza huku huduma za matibabu ya saratani zikipatikana katika hospital ya kanda Bugando na dawa zikipatikana kutoka asilimia 75 na kufikia asilimia 97 kwa kipindi cha miaka minne iliyopita”. Amesema Mhe. Mkalipa.


Sambamba na hayo Mhe. Mkalipa amewataka wananchi Mkoani Mwanza kuendelea kuilinda amani ya Mkoa na nchi kwa ujumla huku wakijitokeza kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwa amani na kuchagua viongozi ambao wataleta maendeleo yenye tija katika taifa na maeneo yao wanayoishi.

Naye Msimamizi wa kituo cha michezo Biro na muandaaji wa tamasha la mbio za pole Bw. Hamisi Bilali amesema lengo kuu la kuandaa tamasha hilo ni kupongeza maendeleo yaliyofanyika ndani ya serikali ya awamu ya Sita katika huduma za afya na kuwahimiza wananchi kutunza afya zao.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema sekta ya afya imeendelea kua bora kwa kutoa huduma za matibabu ya dharura katika hospitali za Halmashauri zote, uboreshaji wa mashine za Xray, CT Scan na utra sound sambamba na hayo serikali imetoa fedha Bilioni 25 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya rufaa katika wilaya ya Ukerewe.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti