• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

DKT. BITEKO ATAKA MIUNDOMBINU YA HOSPITALI YA MISHENI SENGEREMA KUTUNZWA

Posted on: November 1st, 2024

DKT. BITEKO ATAKA MIUNDOMBINU YA HOSPITALI YA MISHENI SENGEREMA KUTUNZWA


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka watumishi wa Hospitali ya Misheni Sengerema na wananchi wa Wilaya hiyo kuhakikisha wanatunza na kulinda vifaa na miundombinu ya jengo la kutolea huduma za upasuaji lililogharimu shilingi bilioni 5.4.

Mhe. Biteko amesema wafadhili waliofadhili mradi wa jengo hilo pamoja na vifaa vyake wanamatumaini makubwa kuwa miundombinu hiyo na vifaa vitatunzwa vizuri ili viweze kutumika kwa muda mrefu.

Naibu Waziri Mkuu ametoa wito huo leo Novemba mosi 2024 wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jengo la upasuaji na mradi wa umeme wa jua (Solar) katika hospitali ya Misheni wilayani Sengerema.

Aidha, Mhe. Dkt. Biteko amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia inathamini sana mchango wa kanisa katika kuboresha huduma za kijamii kama vile Elimu, Afya, na huduma zingine hivyo kuahidi kuendelea kushirikiana katika kuboresha maisha ya wananchi.

Kadhalima Mhe. Naibu Waziri Mkuu ameendelea kuwataka Viongozi wa dini kote nchini kuendelea kuihubiri amani ya nchi yetu ambayo ndio tunu yetu hasa katika kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuhakikisha Watanzania wanabaki kuwa kitu kimoja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema kwa upande wa Sekta ya Afya wao kama Serikali wanajivunia Hospitali, ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando, Hospitali Kongwe ya Misheni ya Wilaya ya Sengerema iliyoanzishwa mwaka 1959 (yenye miaka 65) na vituo vingi vya afya ambavyo kwa hakika vimekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu

Sambamba na hilo RC Mtanda amelihakikishia Kanisa Katoliki kwamba Serikali ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutimiza malengo yake ya kulijenga Kanisa na kuwahudumia watanzania.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo la upasuaji lenye vyumba vinne linaloendeshwa na Shirika la Simba Health Foundation na msaada wa ukarimu kutoka Pharus Foundation ya uholanzi na Wadau wengine, Dkt.Marie Voeten, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo amesema jengo hilo lilianza kujengwa mwaka 2023 na kukamilika mapema Julai 2024 na tayari limeanza kutoa huduma.

Akitoa neno la shukrani Mhashamu Baba Askofu Flavian Matindi Kassala, Askofu wa Jimbo la Geita, amewashukuru wafadhili hao kwa kuhakikisha mradi huo unakamilika na kukubali pia kutenga mfuko maalumu wa msaada wa matibabu kwa wananchi wanaoshindwa kukidhi gharama za matibabu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti