• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

DKT. BITEKO ATOA WITO KWA WAHITIMU CHUO CHA SAUT KUWA WAZALENDO

Posted on: December 16th, 2023

DKT. BITEKO ATOA WITO KWA WAHITIMU CHUO CHA SAUT KUWA WAZALENDO


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe, Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Tanzania kwenda Kusaidia jamii kwa kutumia taaluma zao na kujiepusha na Rushwa ili kusaidia watanzania wasiojiweza na kuwainua kutoka kutoka sehemu walipo.

Dkt. Biteko ametoa wito huo leo tarehe 16 Disemba, 2023 wakati wa Mahafali ya Ishirini na Sita ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino cha Tanzania yaliyofanyika kwenye Uwanja vya Raila Odinga chuoni hapo ambapo kwa nafasi ya Ugeni Rasmi wanafunzi 3066 wamehitimu katika ngazi mbalimbali.

Mhe. Biteko amesema anatamani kuona taaluma zao wanazitumia kwa manufaa ya  kusaidia wenye uhitaji kwenye jamii kwa kutoa ujuzi na ubunifu kwa upendo na kwamba ili kutimiza hilo ni lazima wawe na hofu ya Mungu na wenye kutenda zaidi na sio kulalamika na kujihusisha na matendo ya Rushwa.


"Kusoma kwenu hakutathibitishwa kwa cheti mlicho nacho Mkononi bali kwa athari ya matendo yenu baada ya kuhitimu kule muendako, namna ya kukabiliana na matatizo au jinsi ya kusaidia jamii kupitia taaluma zenu na kwakua kule muendako kuna mapambano basi wenye nguvu watasimama na walio dhaifu wataachwa njiani." Dkt. Biteko.


Akijibu hotuba ya Makamu Mkuu wa chuo hicho, Mhe. Biteko ameahidi kuwa Serikali itarekebisha Barabara za Mitaa ambazo zina makorongo na amebainisha kuwa siku za usoni chuoni hapo zitawekwa taa kwa ajili ya kuweka mazingira salama ya wanafunzi hasa usiku na kwamba Mkandarasi wa Ujenzi huo ameshapatikana.

Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Cha SAUT, Askofu wa Jimbo Katoriki la Geita na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoriki Tanzania, Askofu Flavian Kasala amesema Baraza la Chuo hicho linamshukuru Rais Samia kwa Ulezi wa Vyuo nchini kupitia TCU na Bodi ya Mikopo na anaamini kuwa Viwango vya Udahili na Mikopo kwa wanafunzi itaongezeka ili kuendelea kuboresha Elimu Nchini.


Aidha, ametumia wasaa huo kuwasihi wahitimu kuenenda kimaadili huko waendako kwa mujibu wa walivyolelewa na kwenda kukitangaza Chuo hicho kwa kuwa weledi na wenye ujuzi na ubunifu mkubwa katika kazi na kwamba kwa ambao hawataajiriwa waende wakatunie ujuzi walioupata kufanya kwa vitendo kile walichojifunza.

Balozi Prof. Costa Ricky Mahalu, Makamu Mkuu wa Chuo hicho amebainisha kuwa kwenye Mahafali hayo wamehitimu jumla ya wanafunzi 3066 katika fani mbalimbali katika ngazi za Astashahada hadi Shahada ya Udaktari wa Falsafa ambapo 49% ni wanawake na 51% Wanaume na kwamba Maadili na Taaluma ndio nguzo ya Chuo hicho kwenye kutoa Elimu bora.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti