• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

E-MABORESHO IMEKUJA KIMKAKATI KUMALIZA RUSHWA NCHINI- RAS BALANDYA

Posted on: October 9th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewataka wajumbe wa Kamati za Utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa Kuzuia na kupambana na Rushwa kutumia mfumo wa E-Maboresho kwa ufanisi ili kusaidia kumaliza tatizo la Rushwa nchini.

Ametoa rai hiyo leo tarehe 09 Oktoba, 2025 wakati akifungua mafunzo ya mfumo wa kielektroniki wa utekelezaji wa mkakati wa IV wa kitaifa wa kuzuia na kupambana na Rushwa yaani E-Maboresho katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Amesema, serikali inatamani kuona rushwa imetokomezwa kabisa nchini ili kuhakikisha taifa linasonga mbele kwa mujibu wa katiba ya nchi, hivyo matumizi ya mfumo huo yatawaimarisha wajumbe wa kamati kuweza kuchakata taarifa na kuwasilisha kwa wakati kwa ajili ya hatua zinazofuata.

Aidha, Bw. Balandya amemithilisha uboreshwaji mkubwa wa miradi ya maendeleo katika sekta za miundombinu, Elimu, Maji, Afya, Kilimo, Uchukuzi na Miundombinu na mafanikio ya mikakati ya kupambana na rushwa kwani imeleta matumizi mazuri ya fedha kwenye miradi.

Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka OR Ikulu Bi. Christina Maganga amebainisha kuwa mafunzo hayo ya matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kuzuia Rushwa E-Maboresho yamelenga kuwajengea uwezo Wenyeviti na Makatibu wa Kamati hizo pamoja na Maafisa TEHAMA.

Aidha, amefafanua kuwa mafunzo hayo yalikwishafanyika katika mikoa 17 ukiwemo Mkoa wa Mwanza na kwamba kwa siku mbili hizo yamewakutanisha wajumbe kutoka mikoa ya Mara, Simiyu na Kagera ambao watajengewa uwezo juu ya utumaji wa taarifa za utekelezaji wa kila robo kuhusu masuala ya mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa ili maamuzi yatolewe kwa wakati.


Wakati akijinasibu na uwepo wa vivutio lukuki vya utalii mkoani humo na kuwahamasisha kuvitembelea wawapo kwenye mafunzo hayo, Katibu Tawala amewasihi wajumbe wa mafunzo hayo kuhakikisha wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti