• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

EAC YAJIPANGA KUDHIBITI UHALIFU UKANDA WA ZIWA VICTORIA

Posted on: August 11th, 2025

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Bi. Edith Mwaje (Uganda) amesema jumuiya hiyo itahakikisha mradi wa mawasiliano na uchukuzi katika ziwa victoria unakamilika kwa wakati ili kuwa na kituo imara cha utafutaji, ufuatiliaji na uokozi kwa maslahi ya wavuvi na watumiaji ziwa victoria katika nchi wanachama.

Ametoa kauli hiyo mapema leo tarehe 11 agosti, 2025 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mara baada ya kujitambulisha, kufuatia ziara yake pamoja na ujumbe alioambatana nao ikiwa ni mahususi katika Mradi wa kimataifa wa mawasiliano na uchukuzi katika ziwa victoria pamoja na mingine ya kimkakati.


Bi. Mwaje amesema Wavuvi na wasafirishaji ndani ya ukanda wa ziwa victoria wana haki ya kulindwa wakati wote jambo ambalo jumuiya imelipa kulipaumbele kwa kujenga kituo maalumu pamoja na kuweka boti za kisasa za uokozi na ufuatiliaji pamoja na matibabu ndani ya ziwa hilo.


Aidha, ametumia jukwaa hilo kuwamwagia sifa viongozi wa Mkoa huo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa kwa kuufanya mji nadhifu na wenye miradi kabambe ya kimkakati kama daraja la JP Magufuli ambalo limesaidia kuwaondolea adha ya usafiri wananchi wa ukanda huo.


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa huo Ndugu Balandya Elikana amesema serikali ya Tanzania ni mnufauka mkubwa wa mradi huo kwani utasaidia kuwalinda wavuvi na kuwakamata majangili ndani ya ziwa victoria kwa kulinda vizimba vya ufugaji samaki dhidi ya majangili na maharamia.


Ameongeza kuwa serikali imejiandaa na matunda chanya ya mradi huo kwani ndani ya ziwa victoria kuna miradi lukuki ya uvuvi kama boti za kisasa zilizotolewa kwa wavuvi kwa mkopo ambazo zinazingatia viwango vya kimataifa vya uhifadhi wa mazingira mbavyo vitapata uhakika wa msaada wakati wa majanga.


Aidha, amebainisha kuwa huduma za usafirishaji ndani ya ziwa hilo baina ya mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na nchi rafiki unaendelea kuimarishwa kwani Mamlaka ya Bandari inajenga gati la kisasa lenye uwezo wa kupokea meli kubwa katika bandari za Mwanza Kaskazini na Kemondo na Bukoba ambapo kote ujenzi upo katika hatua za ukamilishaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti