• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ENG. CHAGU AMTAKA MKANDARASI UJENZI HOSPITALI UKEREWE KUEPUSHA GHARAMA ZINAZOEPUKIKA

Posted on: March 15th, 2025

ENG. CHAGU AMTAKA MKANDARASI UJENZI HOSPITALI UKEREWE KUEPUSHA GHARAMA ZINAZOEPUKIKA


Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Chagu Ng'oma amemtaka mkandarasi (Dimetoclasa Real Hope LTD) anayejenga mradi wa hospitali yenye hadhi ya Mkoa wilayani Ukerewe kuepuka gharama zinazoepukika katika utekelezaji wa mradi.

Mhandisi Chagu ametoa agizo hilo mapema leo jumamosi tarehe 15 Machi, 2025 akiwa katika kikao kazi cha tatu cha ufuatiliaji wa utekelezaji wa mradi huo kilichofanyika katika eneo inapojengwa hospitali hiyo katika kijiji cha Bulamba - Nansio wilayani Ukerewe.

Amesema, vitako vya nguzo katika kuandaa msingi ni lazima kwanza wafanye marekebisho madogo kwa maeneo yenye ardhi ngumu inayohusisha mawe kwa kutochimba na kuharibu miamba ili kupunguza gharama za ongezeko la fedha kwa siku za usoni.

"Mkandarasi tangia tarehe 13 Machi, 2025 umeshapewa fedha za awali zaidi ya shilingi Bilioni 3.7 kwa sasa kazi yako ni kuongeza watenda kazi ili ujenzi uende kwa kasi tunayotaka na hadi juni umalize hatua ya msingi." Mhandisi Chagu.

Aidha, ameongeza kuwa huduma za umeme na maji ziko mbioni kufika kwenye eneo hilo kwa ushirikiano baina ya Mkandarasi, msimamizi wa mradi na mamlaka husika ambapo fedha za kulipia kufikisha mtandao zimeshapatikana.

Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba ameongeza kuwa idara ya afya ambao ndio wenye mradi wanatamani ujenzi ukamilike kwa wakati sahihi kwa mujibu wa mkataba ili huduma za kibingwa na bobezi zianze kutolewa kwa wananchi wa visiwani humo.

Naye, Mhandisi John Bhoke kutoka kwa Mkandarasi amebainisha kuwa ujenzi umeanza kwa kasi na majengo yote yatakwenda kwa pamoja kwani tayari maeneo yanayohitajika kuchimbwa kwa ajili ya ujenzi wa msingi kazi hiyo imefanyika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti