• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

FUNGUENI BENKI YENU YA USHIRIKA MAPEMA MUONGEZE MAPATO: RC MAKALLA

Posted on: October 24th, 2023

FUNGUENI BENKI YENU YA USHIRIKA MAPEMA MUONGEZE MAPATO: RC MAKALLA


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija ameishauri Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuharakisha uanzishwaji wa Benki ya Ushirika ili kuwa na chombo imara cha kiuchumi.

Akizungumza Jumatatu hii kwenye viwanja vya Furahisha kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati wa ufunguzi wa wiki ya Vyama vya Ushirika wa akiba na mikopo,amesema hakuna sababu ya kuchelewa kuwa na Benki wakati uwezo wa kuwa na Taasisi hiyo wanao.

"Kisheria  kuwa na Benki lazima uwe na mtaji wa Sh Bilioni 15 lakini najua sasa mmekaribia kufikia kiwango hicho, fanyeni juu chini mfikie malengo hayo ili mjenge chombo imara cha kiuchumi hapa nchini." Ludigija.


Amesema amesikia taarifa ya baadhi ya Saccoss zimekopesha zaidi ya Shs bilioni 100 na nyingine trioni moja ambayo ni ni hatua kubwa sana ya kimaendeleo.

Awali akitoa taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Mwanza, kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Ndg.Daniel Machunda amesema wana jumla ya Saccoss 371 na wanachama 14,638 huku wakiwa na mtaji wa Shs bilioni 12.7.

"Ndugu mgeni rasmi vyama vyetu vya Ushirika wa akiba na mikopo vimekuwa msingi imara wa kuinua vipato vya wananachama wake ambapo kila mwaka mikopo ya Shs bilioni 12.5 hutolewa". Machunda.

Kuhusu maendeleo ya vyama vya Ushirika wa akiba na mikopo nchini, Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Dkt. Benson Ndiege amesema sasa wanataka kutoa wigo zaidi kwa kila mwanachana kuwa na uwezo wa kujiunga na Saccoss nyingi tofauti na sasa kuwa moja pekee.

"Nimetembelea baadhi ya nchi hapa Afrika na Ulaya wenzetu wamepiga hatua zaidi na kuwa na wanachama wengi kutokana na namna walivyoziboresha,ni wajibu wetu kufanya mageuzi hayo",Dkt.Benson

Kilele cha wiki ya Vyama vya Ushirika wa akiba na mikopo ni Oktoba 26 mwaka huu ambapo Tanzania inajumuika na Mataifa mengine ulimwenguni kusheherekea.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti