• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: January 28th, 2026

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza imefanya kikao kazi na viongozi na watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu ujio wa Daftari la Makazi na Bima ya Afya kwa Wote.

Akifungua kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amesema Daftari la Makazi linalenga kuwasajili wananchi wote kwa ngazi ya kaya ili kurahisisha utambuzi na upatikanaji wa huduma za kijamii.

Amesema Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji watakuwa wahusika wakuu wa kusimamia madaftari hayo, huku wananchi wakitakiwa kuhakikisha wanajisajili.

Aidha amesisitiza kuwa ni wakati sasa kwa viongozi na watendaji kwenda kutoa elimu kwa wananchi.

Ndugu Balandya ameongeza kuwa Bima ya Afya kwa Wote tayari imezinduliwa na Waziri wa Afya na kwamba juhudi zinaendelea kuhakikisha wananchi wanapata elimu kuhusu huduma 372 zinazopatikana kuanzia ngazi ya zahanati hadi mkoa kupitia kitita cha jamii.

Kwa upande wake, Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mwanza Bw. Jarlath Mushashu amesema Mkoa ulizindua rasmi uhamasishaji wa elimu ya bima tarehe 17 Desemba, 2025 ili kila mwananchi apate uelewa wa mfuko huo.

Ameeleza kuwa Bima ya Afya kwa Wote itasogeza huduma karibu na wananchi na kuwezesha usajili wa bima kwa makundi mbalimbali ikiwemo kaya na mashirika huku mfumo wa huduma ukiwa ni wa kulipia kabla ya kupata huduma.

Amefafanua kuwa kaya yenye watu kuanzia mmoja hadi sita italipia Tshs. 150,000 kwa mwaka, ambapo wanufaika watasajiliwa kwenye mfumo maalumu unaosomana na mifumo mingine ya Serikali.

Kikao kazi hicho kilichowahusisha Mameya, Wenyeviti, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Maafisa Mipango, Utumishi na Waweka Hazina, pia kimejumuisha mafunzo ya Mpango wa Ufadhili Mbadala unaoratibiwa na Wizara ya Fedha.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti