• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ICGLR Yahitimisha mkutano wake rasmi wa maadhimisho ya 14 kamati ya ukaguzi wa madini

Posted on: September 6th, 2019


Katibu Tawala Mkoa (RAS) Mkoa wa mwanza Christopher Kadio amehitimisha mkutano wa 14 wa kamati ya Ukaguzi wa madini (ICGLR) unao husisha nchi (12) za maziwa makuu, Mkutano huu umefanyika katika hoteli ya Belmont jijini Mwanza kwa lengo la kupambana na uvunaji haramu wa madini ili kuongeza thamani ya madini na kukuza uchumi wa nchi za maziwa makuu.

Akifungua mkutano huo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella Kadio ameupongeza ujio wa wanakamati hao mkoani hapa kwani wameweza kutembelea na kuzitangaza fursa za kitaliii zilizopo mkoani Mwanza pia amewakaribisha kutembelea fursa nyingine za kitalii zilizopo jirani kama Serengeti kwani ujio huu umesaidia kuutangaza mkoa wetu na kukuza uchumi wetu.

“Wageni wetu wamepata fursa pia wasaa wa kuweza kuangalia fursa za kitalii tulizonazo kama kisiwa cha sanane na utalii uliopo pia tumewaambia tuko jirani na maeneo ya utalii kama Serengeti wanaweza pia kuitembelea,” Alisema Kadio.

Aidha Kadio amebainisha kuwa licha ya kujaliwa na Mwenyezi Mungu maliasili nyingi lakini  changamoto imekuwa maliasili tulizojaliwa zinawasaidiaje wananchi wa nchi zetu, pia amepongeza lengo la kamati hiyo kwani itasaidia kuhakikisha maliasili zinavunwa kwa njia sahihi na kuleta faida kwa wananchi wake.

“Nchi hizi zimejaliwa na Mwenyezi Mungu kuwa na maliasili nyingi lakini changamoto imekuwa maliasili tulizojaliwa zinawasaidiaje wananchi wa nchi zetu pia tunashukuru kwamba hii kamati ya ukaguzi inafanya sehemu yake katika kuangalia na kuhakikisha kuwa maliasili hizi zinapovunwa biashara hii ikiwa wazi tunaweza kuona wananchi wanapata faida katika biashara hii,” Alisema Kadio.

Naye Katibu Mkuu wa kamati hiyo Mhe. Barozi Zackary Muburi Muita ameweza kubainisha matokeo ya uvunaji haramu wa madini kwani unachangia vita na serikali kukosa mapato ya miradi ya wananchi wake.

“Sababu ya uvunaji haramu wa maliasili unachangia sana vurugu, vita na serikali kukosa utajiri wa miradi ya wananchi hasa madini,” Alisema Muita.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Fr. David Ngoy Luhaka amesema wameweza kuzindua kitabu kipya cha kamati hiyo kitakacho angalia madini yanachunguzwa katika njia ya uwazi na kusema kitabu hicho kipo wazi kwa kila mwanachama wa jumuiya hiyo.

“Tumeanzisha kitabu kipya kitakacho toa nafasi kwa wanachama wake wenye kampuni la ukaguzi wa madini kujiorodhesha ili kuwe na ukaguzi wa mara kwa mara” Alisema Luhaka.

Aidha ametoa wito kwa nchi zote za Maziwa makuu ambazo hazijajiunga na kamati hiyo kuwa zinakaribishwa na mlango upo wazi kwani lengo kubwa ni kuhakikisha madini yetu yanathaminiwa katika hali nzuri.

“Niwatake kuwa nchi zinazotaka kuungana nasi katika uchunguzi mlango upo wazi hata kama kuna nchi mbalimbali waje kwa sababu tunapenda wote walio katika nchi za maziwa makuu ili madini yetu yathaminiwe katika hali nzuri,” Alisema Luhaka.

Hata hivyo Kadio ametoa ushauri kwa washiriki wa kikao hicho kwa kuwashauri pia kuwa waadilifu katika kamati hiyo ya ukaguzi kwani watasaidia katika kupiga hatua kwenye sekta hii ya madini lakini pia amewatia moyo kwa kazi kubwa wanayoifanya kwa ajili ya maendeleo ya nchi zetu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti