• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ILEMELA YANG’ARA UBORESHAJI LISHE YA WANAFUNZI KUPITIA URUTUBISHAJI VYAKULA

Posted on: August 26th, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Bw. Ismail Ali Ussi ameipongeza Halmashauri Manispaa ya Ilemela kwa kusimamia vema afua za lishe katika kuhakikisha wanafunzi wanapata vyakula vyenye virutubishi vinavyowasaidia kujenga afya bora wawapo shule.

Bwana Ussi ametoa pongezi hizo leo Agosti 26, 2025 wakati akikagua shughuli za usindikaji na uongezaji wa virutubishi  kwenye ungalishe katika kiwanda cha Kipipa Limited kilichopo mtaa wa Sabasaba chenye thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 1.2.

Amesema, viongozi wa Halmashuri hiyo wameonesha kwa vitendo kiu ya kuwalinda watoto na udumavu na utapiamlo kwani kwa kushirikiana na kiwanda hicho wanapeleka shuleni asilimia 18 ya bidhaa za vyakula zinazozalishwa kiwandani hapo.

“Ombi langu kwa wakulima na wafanya biashara kuunga mkono juhudi za serikali na kwa wanaomsimamia mwekezaji huyu kuchakata na kuzalisha bidhaa mbalimbali za nafaka kama mtama, mahindi na mhogo kwa kununua na kuwapatia watoto pamoja na wenye mahitaji maalum.” Amesema Bw. Ussi.

Aidha, amewapongeza wawekezaji hao kwa kubuni mradi mzuri ambao umezaa matunda ya uzalishaji wa tani 36.5 za nafaka na 5 za muhogo kwa mwezi na ametoa wito kwa Taasisi za kifedha kuendelea kuwatia moyo wawekezaji wa aina hiyo yenye tija ikiwemo Benki ya kilimo ambayo awali imewakopesha zaidi ya milioni 800.

Awali, Mwenge wa Uhuru umekagua mradi wa Kikundi cha Cross Over katika mtaa wa furahisha kabla ya uzindua malori 2 na kijiko kimoja mahsusi kwa ajili ya kuzolea taka kwenye Soko la kimataifa la Samaki Mwaloni pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari ya Ilemela.

Vilevile, mwenge wa uhuru umezindua ofisi ya kata Nyasaka pamoja na mradi wa jengo la mama na mtoto katika zahanati ya Nyakato kabla ya kuzindua huduma ya matumizi ya nishati safi katika shule ya sekondari Buswelu na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti