• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Jaji mstaafu Thomas Mihayo kuongoza kamati ya uchunguzi ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Ukerewe

Posted on: December 21st, 2022


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ameunda kamati ya watu watano itakayoongozwa na Jaji Mstaafu Thomas Mihayo kufanya Uchunguzi kwenye utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa inayojengwa wilayani Ukerewe kufuatia malalamiko ya uwepo wa ubadhirifu wa fedha kwenye mradi huo.

Waziri Ummy amebainisha hayo leo jumatano disemba 21, 2022 wakati wa ziara yake Wilayani Ukerewe alipofika kukagua mwenendo wa ujenzi wa mradi huo kufuatia agizo la Mhe. Makamu wa Rais alipofanya ziara yake wilayani humo Novemba 25, 2022 na kumtaka Waziri wa Afya kufika kukagua mwenendo wa Ujenzi kutokana na malalamiko ya wananchi.

"Niseme wazi, kwa macho mimi nimeona kuwa gharama za Ujenzi kwenye mradi huu zipo juu na haziendani kabisa na thamani ya fedha zilizolipwa hakuna Bilioni 2.9 pale, hivyo naunda timu yangu ambayo itaongozwa na Jaji Mstaafu Thomas Mihayo ambayo itachunguza malalamiko ya wananchi wa Ukerewe kwenye mradi wao." Mhe. Ummy.

Amefafanua kuwa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Mkoa Ukerewe uliasisiwa na Mhe. Waziri Mkuu alipofika wilayani humo na kubaini uhitaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ili wananchi wa Ukerewe wasisafiri tena kwenda Sekou Toure au Bugando lakini watekelezaji wameamua kuiboresha hospitali ya Wilaya badala ya kujenga hospitali mpya ambayo ingejumuisha huduma za kibingwa za matibabu zinazoendana na miundombinu.

"Kama hili jengo la Kliniki ya Mama na Mtoto ni lanini hapa wakati hata kwenye Hospitali zingine tunaziondoa, hamjanishawishi kuwa baada ya Ujenzi huu wanaukerewe watapata huduma za kibingwa hapa hivyo hatujatatua tatizo maana huduma zinazotolewa hapa bado zipo kwenye Hospitali ya Wilaya ambayo inatumika na mwanamke ambaye atafika hapa na matatizo makubwa ya uzazi bado hatosaidiwa hivyo ni lazima tutafakari hilo na tujielekeze huko." Mhe. Waziri amefafanua.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema kuwa kumekua na makosa tangia hatua za awali katika utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo kwa kutofuata taratibu za malipo, kutekelezwa kwa kuchelewa na miundombinu kutozingatia mahitaji halisi ya wananchi kwenye huduma za kibingwa.

"Rais Samia hata ukimwangalia machoni anaonesha ana dhamira ya dhati ya kutaka wananchi wake wapate huduma za kijamii na ndio maana analeta fedha kwenye miradi hivyo basi ni wajibu wetu kutekeleza miradi kwa mujibu wa sheria na wizara yetu haipo tayari kuona mtu hatimizi wajibu wake pasipo kuchukuliwa hatua." Mhe. David Silinde, Naibu Waziri TAMISEMl.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalage alifafanua kuwa baada ya Serikali kuona jiografia ya Kisiwa hicho na mahitaji kuwa makubwa ni vema ikipandishwa hadhi kuwa ya Rufaa ya Mkoa ndipo Mhe. Rais alitoa Shilingi Bilioni 2.69  kwa ajili ya kuanza ujenzi ambapo kwa sasa umefikia asilimia 62 ya utekelezaji.

Mbunge wa Jimbo la Ukerewe Mhe. Joseph Mkundi amesema kwenye utekelezaji wa mradi huo wananchi wa Ukerewe wanakwazwa na mpango wa Miundombinu ya majengo, ucheleweshaji wa Ujenzi huo na thamani ya mradi kuonekana kuwa chini ya fedha zilizolipwa kwa Mkandarasi na ametoa wito kwa wizara kusaidia kupata suluhu ya jambo hilo ili mradi ukamilike.

"Katika wilaya yetu ya Ukerewe tuna visiwa 38 wananchi na wanawake wenzangu kwenye visiwa hivyo wanapata shida sana ya huduma za uzazi, nikuombe tupate vituo vya afya kwenye visiwa vikubwa ili wananchi walio wengi wapate huduma za Afya bila kusafiri umbali mrefu kuja kwenye Hospitali ya wilaya." Mhe. Furaha Matondo, Mbunge viti Maalum.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti