• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

JIJI LA MWANZA LAJIELEKEZA KWENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI WAJENGA MADARASA MFUMO WA GHOROFA

Posted on: July 15th, 2023

JIJI LA MWANZA LAJIELEKEZA KWENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI WAJENGA MADARASA MFUMO WA GHOROFA


Halmashauri ya Jiji la Mwanza yakamalisha Ujenzi wa Madarasa 12 kati ya 16 kwa mfumo wa ghorofa kwenye Shule ya Sekondari ya Mirongo kwa gharama za zaidi ya Sh Milioni 513.5 kutoka vyanzo vya Mpango wa Ustawi wa Taifa na Kuthibiti Uviko 19, mapato ya ndani ya Halmashauri na Serikali kuu.

Hayo yamebainishwa leo julai 15, 2023 wakati Mwenge wa Uhuru ulipofika kuzindua madarasa 12 yaliyokamilika kwa awamu ya kwanza yakiwa na samani ambayo yatasaidia   kuondoa msongamano wa wanafunzi darasani kwani yana uwezo wa kuchukua wanafunzi 600.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa madarasa hayo, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kujenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa ambapo yatasaidia kupunguza gharama za ujenzi kutokana na kutumia ardhi ndogo tofauti na endapo wangejenga kwa mfumo wa kawaida.

"Baada ya kukagua nyaraka na ujenzi kwa ujumla, Mwenge wa uhuru umeridhika na ubora na ndani ya siku tano naomba tuyafanyie kazi mapungufu hasa kwenye upande wa viti na meza ili vijana wapate elimu kwenye mazingira bora kabisa kama Mhe. Rais alivyoweka nia hiyo." Ndugu. Kaim.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyamaganawa Mhe. Amina Makilagi amefafanua kuwa kwa sasa wanafunzi watakaa kwa uwiano wa 50 kwa darasa tofauti na hali ilivyokua ambapo walilazimika kuketi wanafunzi 100 ndani ya chumba cha darasa jambo ambalo lilipelekea kuwa na mazingira magumu ya ufundishaji na kujifunzia kwa wanafunzi na walimu.

"Miaka 2 nyuma shule za ghorofa jijini Mwanza zilikua tatu tu lakini ndani ya Miaka Miwili ya Rais Samia tumejenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa kwenye shule 13, achilia hapa lakini pale bugarika pakikamilika tutakua na madarasa 16, Mkolani, Mandu na Mkuyuni madarasa 24 kwa mfumo huu kwakweli tuwapongeze wote waliosimamia miradi hii." Mhe. Makilagi.

Awali taarifa ya radi huo iliyosomwa kwa mkimbiza Mwenge wa Uhuru ilifafanua kuwa uamuzi kwa Ujenzi wa madarasa hayo kwa mfumo wa ghorofa umetokana na hali ya ongezeko la watu na ufinyu wa ardhi na kwamba kwa ujenzi wa madarasa hayo 16 umeokoa eneo la ardhi la mita za mraba 656 na kwamba fedha zaidi ya milioni 88 zimeokolewa kwenye ardhi.

Mapema asubuhi, Mwenge wa Uhuru umekabidhi mifuko 300 ya saruji kwenye shule ya msingi Samia ambayo yatasaidia katika Ujenzi wa madarasa 10 yaliyoanzishwa na wananchi na baadae ukaangazia kwenye upande wa Sekta ya utawala ambapo umefanyika uzinduzi wa ofisi ya kata ya Mabatini.

Vilevile, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Unguja A kwa kiwango cha lami yenye urefu kwa mita 372 kwa gharama ya milioni 348.1 na kuagiza usimamizi mzuri ili ikamilike kwa ubora na wananchi wakatakiwa kutofanya biashara barabarani na kuhakikisha wanaitunza Miundombinu hiyo.

Kabla ya Mwenge wa Uhuru kufungua mradi wa ujenzi wa wa Miundombinu katika kituo cha afya Bulale na kuagiza urekebishaji wa mifumo ya maji na kutenganisha taa na feni ili mwanga usiwe na mawimbi, mwenge wa uhuru umeweka jiwe la nsingi kwenye jengo la uwekezaji la Family Corner linalojihusisha na makazi (Apartments).

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti