• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

KANDA YA ZIWA YAPIGWA MSASA UWEKEZAJI, DIRA YA TAIFA 2050 YATAJWA MSINGI WA MAPINDUZI YA UCHUMI

Posted on: February 4th, 2026

Serikali imeeleza kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyozinduliwa rasmi mwaka 2025, unaweka mkazo mkubwa katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tatu bora Afrika kwa kuvutia mitaji, huku mikoa ya Kanda ya Ziwa ikitajwa kuwa nguzo muhimu ya safari hiyo ya mageuzi ya uchumi.

Hayo yamesemwa Jijini Mwanza na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (MB), wakati wa Kongamano la Uwekezaji kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa, lililoandaliwa kama sehemu ya Kampeni ya Kitaifa ya Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani yenye lengo la kuchochea ushiriki mpana wa Watanzania katika uwekezaji.

Mhe. Kapinga amesema uwekezaji ni nyenzo muhimu ya kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi kwa kuvutia mitaji, kuleta teknolojia ya kisasa, kuongeza ajira kwa vijana, kukuza ujuzi wa rasilimali watu, kuongeza mapato ya kodi na yasiyo ya kodi, kuongeza uzalishaji wa bidhaa na kuokoa fedha za kigeni zinazotumika kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.

Amefafanua kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kujenga Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea, kupitia nguzo tatu na vichocheo vitano, huku nguzo ya kwanza ikilenga kujenga uchumi imara, jumuishi na shindani kwa kuimarisha mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji.

Ameitaja Taasisi ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kama mhimili mkuu wa utekelezaji wa Dira 2050 katika eneo la uwekezaji, akisema taasisi hiyo ndiyo mtafsiri wa maono ya Taifa kwa vitendo, kufuatia kuunganishwa kwa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mamlaka ya Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) chini ya Sheria ya mwaka 2025.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema utekelezaji wa kampeni hiyo katika Kanda ya Ziwa utaongeza kasi ya uwekezaji wa ndani, akibainisha kuwa mikoa ya kanda hiyo inachangia takribani asilimia 25 ya Pato la Taifa, hivyo miradi ya uwekezaji itakayotekelezwa itaongeza zaidi mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti