• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

KUFUATIA MTAALA MPYA RAS MWANZA ATOA MAAGIZO KWA WATENDAJI SEKTA YA ELIMU

Posted on: February 5th, 2025

KUFUATIA MTAALA MPYA RAS MWANZA ATOA MAAGIZO KWA WATENDAJI SEKTA YA ELIMU


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amewataka watendaji sekta ya elimu kuhakikisha wanabadilika na kujifunza namna ya kutekeleza mtaala mpya ulioboreshwa ili waweze kuelewa na kutekeleza mabadiliko hayo yaliyoanza kutumika Januari 2025 kwa ufanisi katika Shule zao.

Ametoa agizo hilo mapema leo Jumatano Februari 05, 2025 Wilayani Sengerema wakati akifungua kikao cha Maafisa Elimu na wadhibiti ubora walioketi kutathmini utekelezaji wa shughuli za Elimu kwa mwaka 2024 na kuweka malengo ya kufanya vizuri zaidi.

Aidha, RAS Balandya amewataka kutathmini ubora na udhaifu wao na kuweka mikakati bora ya kufanya vizuri zaidi na kwamba wasibweteke kwa kuwa Mwanza imefanya vizuri kitaaluma katika mitihani yote hususani wa kidato cha nne ambapo ufaulu ni wa 98.2%.

Ili kuendelea kuwa bora, Ndg. Balandya amewataka wataalamu hao kuweka mikakati ya namna ya kukabili changamoto zinazorudisha taaluma nyuma kama wanafunzi kumudu stadi za kusoma, kuhesabu na kuandika pamoja na ufundishaji duni ili kubaki juu kitaaluma.

Pia amewataka maafisa hao kuweka mpango wa kufanikisha Mkoa kufanya vizuri zaidi  kwenye michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA 2025 na kuendelea kusimamia fedha za ujenzi wa miundombinu bora ya elimu ambapo amebainisha kuwa mwaka 2024 Elimu Msingi imepokea zaidi ya Bilioni 24 na kwa sekondari Bilioni 17.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Mwalimu Martin Nkwabi amebainisha kuwa 2024 ulikua mwaka mzuri mathalani katika uboreshaji miundombinu, taaluma kwa mitihani ya upimaji na mitihani ya Taifa na hata katika michezo kwani Mwanza imeibuka kidedea.

Vilevile, amesema kiwango cha kuweka wanafunzi shuleni kimepanda kutoka 7% mwaka 2023 hadi 4% mwaka 2024 hivyo kiwango cha kuwafanya wanafunzi wadumu darasani ni kikubwa na kimefuta mdondoko.

Ujio wa mtaala mpya ulioboreshwa ni katika kutekeleza agizo la Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuboresha mitaala ya Elimu Msingi, Sekondari na Ualimu ili kuwawezesha wahitimu kuwa na ujuzi wa kujiajiri na kuajiriwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti