• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MADAKTARI BINGWA KUWEKA KAMBI YA MATIBABU SIKU 5 MWANZA

Posted on: October 20th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amepokea madaktari bingwa na bobezi 58 wa Mama Samia wa awamu ya nne kutoka katika kada sita ambao wamekuja kuweka kambi za matibabu katika Hospitali za Wilaya na Halmashauri 8 za Mkoa huo.

Madaktari hao wataweka kambi Mkoani Mwanza kuanzia tarehe 20 hadi 24 Oktoba 2025 wakitarajiwa kutoa huduma za Ubingwa katika maeneo ya magonjwa ya ndani, wanawake na ukunga, upasuaji, ubobezi kwa watoto wachanga, ubingwa katika huduma za kinywa na meno, usingizi na ganzi, pamoja na huduma za ubingwa na ubobezi katika uuguzi.

 

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kambi hiyo Bw. Balandya amesema ujio wa madaktari hao bingwa ni wa faida kwa watumishi wa idara ya afya pamoja na wananchi kwani utasaidia katika kutoa elimu, mafunzo na huduma.

“Naamini kwamba ujio wenu katika Mkoa wa Mwanza utasaidia kukuza ujuzi wa hawa wenzetu waliopo katika Mkoa huu ili waweze kuondokana au kupunguza changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao ya kazi”. Amesema Bw. Balandya.

Aidha, amewahakikishia wataalamu hao kupata ushirikiano kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri kwa kipindi chote ambacho watakua wameweka kambi Mkoani humo, huku akiwakaribisha wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kupatiwa matibabu.

Vilevile, Katibu Tawala ametumia wasaa huo kuishukuru serikali kwa kuwaletea wataalamu hao huku akibainisha kuwa mara zote imekua ikihakikisha inaboresha huduma na miundombinu mkoani humo na akazitaja Bilioni 63 zilizotolewa kwa ajili ya kuboresha miundombinu na vifaa tiba kwa kipindi cha miaka 4.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewasisitiza madaktari hao bingwa kwenda kubadilishana ujuzi na madaktari ambao watawakuta katika hospitali za Wilaya.

Msimamizi wa timu hiyo kutoka Wizara ya Afya Bi. Fidea Obimbo amesema lengo kubwa la kambi ya madaktari bingwa na bobezi kufika Mkoani Mwanza ni kuwafikia wananchi kwa huduma tofauti ambazo zilikua ni ngumu kwao kuwafikia.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti