• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Madalali wa Madini watakiwa kutoyatorosha ili kukuza Uchumi wa Nchi

Posted on: July 13th, 2022



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa rai kwa Chama cha Madalali wa Madini Nchini (CHAMMATA) kuthibiti wafanyabiashara wa Madini, Vito na Chuma kuacha utoroshaji wa Madini ili kuimarisha ukusanyaji wa maduhuli na kuweza kuyafikia malengo ya Wizara ya makusanyo kupitia sekta hiyo.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo wa kizalendo leo Julai 13, 2022 wakati wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Madalali wa Madini Tanzania (CHAMMATA) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya Waziri wa Madini Mhe. Dkt Dotto Biteko.

Aidha, amewapongeza chama hicho kwa kupata usajiri na amewaahidi kuwa Seriikali kupitia Wizara ya Madini itaendelea kushirikiana nao ikiwa ni pamoja na kufuatilia kwa karibu suala la kufanya biashara za Madini kwa kutumia leseni ya aina moja kokote nchini ili kulipatia ufumbuzi suala hilo katika kuboresha sekta hiyo .

Akiongea kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Emil Kasagara amewapongeza CHAMMATA na amewaalika kushiriki Maonesho ya Kilimo, Mifugo na Biashara Kanda ya Ziwa Magharibi yatakatofanyika kwenye viwanja vya Nyamhongolo kuanzia Agosti 1-8, 2022.

Mwenyekiti wa CHAMMATA Ndugu Jeremia Simon ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Madini kwa kuanzisha mfumo wa Masoko rasmi ya Madini ambayo yameleta Maendeleo makubwa kutokana na kuondokana na biashara holela ya madini na wameachana na kutembea na fedha nyingi hali iliyokua inahatarisha usalama wao.

"Mfanyabiashara yeyote wa Madini atakayetorosha Madini, Chama (CHAMMATA) kitachukua hatua kali kwake ikiwa ni pamoja na kuishauri Tume ya Madini kumnyang'anya Leseni mfanyabiashara huyo na kuhakikisha hafanyi tena biashara ya Madini nchini" amefafanua Mwenyekiti.

Aidha, amefafanua kuwa malengo ya kuanzisha Chama cha Madalali wa Madini Tanzania (CHAMMATA) ni kuwa na daraja la kuwaunganisha wafanyabiashara na serikali kupitia taasisi zake kama Tume ya Madini ikiwa ni pamoja na kutetea na kusimamia haki za wafanyabiashara wa Madini, vito na Chuma.

"Madalali ni daraja la kuunganisha wachimbaji wa Madini na wauzaji wakubwa, ni watu muhimu sana nasi kama Tume ya Madini tunawathamini na kuwapenda mno hivyo tunaomba msimamie kanuni na Malengo mliyoridhia kwenye Katiba yenu ili Msaidie Utoroshaji wa Madini nchini." afisa Madini Mkazi Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Nyaisara Mgaya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti