• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Madereva Waaswa kuthamini Afya zao

Posted on: July 2nd, 2018


Madereva daladala na makondakta watakiwa kuthamini afya zao kwa kuona umuhimu wa kuwa na bima ya afya na kunufaika na huduma bora za matibabu kwa gharama nafuu ili kuendelea kuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa bidii na kuchangia uchumi wa familia zao na Taifa.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mary Tesha kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella wakati akikabidhi kadi za bima ya afya kupitia mfuko wa NHIF kwa wanachama wa Chama cha Madereva na Makondakta wa Daladala Mkoa wa Mwanza (MWAREDDA).

Alisema Taifa linahitaji watu wenye afya ili kufanya mambo ya kimaendeleo hivyo ni bora kutokusubili mpaka kuugua jambo la msingi ni kupima na kuanza matibabu kabla ugonjwa haujawa mkubwa hiyo itasaidia kuepukana na vifo vya gafla .

"Watu wote tupo kwenye hatari ya kupata ajali lakini hili kundi lenu lipo kwenye hatari zaidi kwa sababu muda mwingi mpo barabarani hivyo bima ya afya ni muhimu pindi upatapo ajali upate matibabu bure nasikia kuna watu wanafia kwenye gari wakiwa wanaendesha hiyo kwa sababu hakujua kama anaumwa na inatokana na kutokupima na kutojihusisha na masuala ya afya,"alisemaTesha.

Naye Mwenyekiti Msaidizi MWAREDDA Ezekiel Lameck alisema wao wapo tayari kuwekeza kwenye afya japo kuwa vipato vyao siyo vya kuridhisha lakini wanatambua kuwa bila ya kuwa na afya bora hawataweza kumudu kazi yoyote na kuwa rahisi zaidi kupoteza maisha .

Aliongeza kuwa chama hicho kilianzishwa mwaka jana kikiwa na wanachama 50 ambapo hadi sasa kina wanachama 320 hivyo lengo ni kuhakikisha wanachama wote wanajiunga na mfuko wa NHIF ili kuondokana na adha ya kupata huduma za matibabu.

“Lengo la kuanzishwa kwa chama hiki ni kutetea haki na wajibu wa madereva na makondakta katika kazi zao, kutoa elimu na kuwajengea uwezo ili waweze kumudu vyema majukumu yao kwa mjibu wa sheria za nchi hususani sheria za usalama barabarani pamoja na kupigania mazingira bora ya kazi zao,”alisema Lameck.

Kwa upande wake Kaimu Meneja mfuko wa NHIF Mkoa wa Mwanza, Calystus Mpangala amesema kwa mwaka wa fedha 2017/18 malengo yalikuwa kusajili wajasiriamali 1200 Mkoani Mwanza kupitia mpango wa KIKOA ambapo hadi sasa umevuka lengo kwa kusajili wajasiriamali 1,223 hii ikiwa ni sawa na asilimia 102.

Aliongeza mfuko wa bima ya afya umedhamiria kumfikia kila mtanzania hivyo bodi imeridhia kuwa na utaratibu wa utoaji huduma za matibabu kwa kadi kwa vikundi ama ushirika vilivyo katika sekta isiyo rasmi kama mama lishe,AMCOS, SACCOS, VICOBA, umoja wa bodaboda na daladala na kundi la ujasiliamali ambao hawawezi kugharamia matibabu kama watu binafsi.







Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti