• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

Posted on: February 2nd, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefungua rasmi mafunzo ya awamu ya kwanza kwa Waheshimiwa Madiwani waliochaguliwa katika Uchaguzi wa Oktoba 2025 kutoka Halmashauri za Jiji la Mwanza, Manispaa ya Ilemela, pamoja na Halmashauri za Magu na Ukerewe.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mhe. Mtanda amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo madiwani katika maeneo ya msingi ikiwemo uongozi na utawala bora, sheria za uendeshaji wa serikali za mitaa, uendeshaji wa vikao vya kisheria, uandaaji wa mipango, bajeti, pamoja na usimamizi wa watumishi na miradi ya maendeleo.

Amesisitiza kuwa bado kuna dhana potofu miongoni mwa viongozi na wananchi kuwa usimamizi wa miradi ni jukumu la Wakuu wa Mikoa au Wilaya pekee hali inayosababisha baadhi ya miradi ya maendeleo kutotekelezwa ipasavyo, huku madiwani wakidhani ni jukumu la wahandisi au wakurugenzi.

Mhe. Mtanda amewahimiza Madiwani kutambua kuwa utekelezaji wa miradi katika maeneo yao ndiyo msingi wa uaminifu wao kwa wananchi, akisisitiza umuhimu wa kusimamia miradi, kutoa taarifa pale panapobainika dosari, na kuhakikisha fedha za maendeleo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Pia ametoa wito kwa Wakufunzi kuweka kipengele cha uelewa wa mahusiano kati ya Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa, pamoja na mipaka ya majukumu kati ya madiwani na watendaji wa serikali katika ngazi ya kata, ili kuepusha migongano na kuimarisha utendaji kazi wa pamoja.

Kwa mujibu wa Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, mafunzo hayo yatatolewa kwa muda wa siku tatu na yatahusisha mada 11, zikiwemo uongozi na utawala bora, muundo na madaraka ya serikali za mitaa, pamoja na uendeshaji wa vikao na mikutano ya kisheria.

Mada za mipango, bajeti, usimamizi wa miradi na udhibiti wa fedha zinalenga kuwajengea madiwani uwezo wa kusimamia rasilimali za umma kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda ametoa maelekezo kwa Halmashauri ambazo bado hazijafikia kiwango cha asilimia 80 ya matumizi ya mashine za POS, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, kukamilisha ununuzi wa mashine hizo ndani ya miezi mitatu na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti