• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Makarani wa Sensa Mwanza wafanya zoezi la majaribio

Posted on: August 12th, 2022


Makarani wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoani Mwanza leo Agosti 11, 2022 wamefanya mafunzo kwa vitendo kwaajiri ya  kutambua mipaka na kuhoji wanakaya kwa majaribio katika maeneo mbalimbali huku wakitumia Madodoso yaliyopo kwenye Vishikwambi.

Mkufunzi wa Mafunzo ya Sensa ngazi ya Mkoa kutoka kituo cha Maliasili, Sambona Peres amesema katika kituo chao wamewaandaa Makarani kuwa mabalozi kwa wananch kwa kuelimisha jamii juu ya zoezi hilo ili siku ya Sensa zipatikane takwimu sahihi.

Wakizungumza katika nyakati tofauti Makarani hao wamesema wapo tayari kwa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kwani wamepatiwa mafunzo bora ya kuwawezesha kufanikisha zoezi hilo linalotarajiwa kufanyika jumanne ya Agosti 23, 2022 nchini.

Innocent Mijaya, Mwenyekiti wa Mafunzi Butimba amesema zoezi la dodoso la mipaka na sensa kwa mafunzo ni la siku moja na baadae watarudi tena kwa zoezi la kudodosa dodoso la majengo na kwamba kwa kutumia vishikwambi karani anaonekana amepita kwenye mipaka gani na nini amehoji.

"Kwa takribani siku 12 tumepata mafunzo ya nadharia darasani na sasa tupo katika mafunzo ya uwandani ambapo moja ya kazi ya karani ni kutambua mipaka kabla ya zoezi la kudodosa wanakaya waliopo ndani ya mipaka yake, na ndiyo kazi leo tunayofanya". Amesema Innocent.

Naye, Karani Joyce Ndomaa amejinasibu kuwa kwa kupitia mafunzo hayo ya vitendo wamekagua mipaka ya eneo la ziwa namba 2 Butimna na kwamba zoezi hilo la vitendo limewasaidia kuelewa zaidi kufuatana na mafunzo waliopewa darasani.


"Kwa sasa watu wanashangaa hivi tulivyoshika ni vitu gani, nasi tunaanza kuwaelimisha kuwa vifaa hivi ni vya kazi gani na tunawashukuru Wenyeviti wa mitaa na watendaji ambao wanatusaidia sana kufanikisha zoezi hili." Amesema Nyanda Patrick ambaye ni Karani kutoka darasa la Butimba.

Karani Mary Nyirenda ametoa rai kwa viongozi wa Serikali za Mitaa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa zoezi la Sensa ya watu na makazi huku akibainisha kuwa kwenye eneo la Kawekamo wamekutana na changamoto kama za wanakaya kutokubali kuzungumza, kukataa kuhojiwa na kupelekea kupata taarifa zisizo sahihi kwa baadhi ya kaya hali ambayo inasababishwa na kutowakuta wakuu wa kaya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti