• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

Posted on: April 29th, 2025

MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA


Itakumbukwa mnamo machi 16 na machi 26, 2025 Makundi mawili ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza walikwenda kufanya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Ngorongoro, Hifadhi ya Taifa ya Mwl. Nyerere, Mradi wa kimkakati wa kufua umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) na Mradi wa reli ya kisasa kutoka Mkoa wa Dar es Salaam kwenda Dodoma.

Leo Aprili 29, 2025 makundi hayo mawili kwa uwakilishi yamewasilisha neno la shukrani na zawadi kadhaa Ofisini kwa Mratibu na Muasisi wa Ziara hizo ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana.

Akizungumza ofisini kwa Katibu Tawala, Kiongozi wa Kundi la JNHPP Bw. Paulo Cheyo amesema ilikua ni wasaa mzuri sana kutembelea mradi wa kimkakati wa JNHPP na wameweza kujifunza mengi na kumtakia kila la kheri KIongozi huyo mwenye maono mema kwa Watumishi wake.

“Hakika safari yetu ilikua nzuri na yenye mafunzo, Binafsi sikuwahi kufikiria kufika kutazama uwekezaji mkubwa uliofanywa katika bwawa la Mwl. Nyerere, Ninakushuru sana Kiongozi kwa jitihada zako”. Amesema Bw. Mangabe Mnilago.

Naye Kiongozi wa Kundi la Ngorongoro - Serengeti Bw. Credo Lugaila amesema ziara hizo pia zimesaidia kuwachangamsha na kuleta ari ya ufanyaji kazi, lakini pia amesema imesaidia kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Watumishi na Viongozi wa Mkoa.

“Maneno Matakatifu ya Biblia yanasema upendo wa ndugu na udumu, Tunakushuru sana Baba kwa upendo wako, umethibitisha maana halisi ya Kiongozi anaejali na kuwathamini Watumishi wake, Tunakushuru sana. Amesema Bi. Ine Sibale

Akihitimisha kutoa shukrani hizo Bi. Zawadi Kalilo amesema upendo wa Katibu Tawala ni kama upendo wa Baba lakini kwa Kiongozi huyo kwa Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amekuwa kama “Daddy”. (Akimaanisha mwenye upendo uliokithiri).

Akizungumza mara baada ya kupokea salamu hizo, Katibu Tawala Bw. Balandya Elikana amewashukuru kwa maneno mazuri ya faraja pamoja na maombi na amewataka sasa kwenda kuchapa kazi kwa ufanisi na weledi.

Makundi hayo mawili yamewawakilisha wale Watumishi waliopata wasaa wa kufanya utalii na wamemzawadia kiongozi huyo zawadi mbalimbali ikiwa ni kitambua mchango wake katika kuwathamini Watumishi hao na kwake ikawe kumbukumbu halisi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti