• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MAMLAKA ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA ZATAKIWA KUTOA TAARIFA ZITAKAZOWASAIDIA WANANCHI KUJIEPUSHA NA MAJANGA

Posted on: August 26th, 2024

MAMLAKA ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA ZATAKIWA KUTOA TAARIFA ZITAKAZOWASAIDIA WANANCHI KUJIEPUSHA NA MAJANGA


Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa ametoa wito kwa Mamlaka za hali ya hewa barani Afrika kutoa taarifa sahihi za hali ya hewa hususani za rada ili kuwaepusha wakulima, wavuvi na wananchi na majanga yanayoepukika.

Waziri Mbarawa ametoa wito huo mapema leo Agosti 26, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku 5 kwa Mataifa 13 kutoka barani Afrika yaliyodhaminiwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) yanayofanyika kwenye hoteli ya Malaika Mkoani Mwanza.

Prof. Mbarawa amesema, tahadhari kutoka mamlaka za hali ya hewa hususani za rada zinategemewa sana na wananchi wanaojihusisha na shughuli za uvuvi na kilimo ambao wanahitaji kujua wanapoamka asubuhi watakua na hali gani itakayowaruhusu kwenda kwenye shughuli zao.

"Ninayo imani kuwa kupitia mafunzo haya washiriki wataimarika kwenye utumiaji wa teknolojia na utoaji wa taarifa sahihi za hali ya hewa hususani za rada na itasaidia kuinua uchumi wa nchi na kuiepusha jamii na majanga kama ya kimbunga kwenye maziwa na bahari kwa wavuvi." Amesema Prof Mbarawa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bwana Balandya Elikana amewataka nchi washiriki wa mafunzo hayo kutumia mafunzo hayo kuboresha huduma kwenye mamlaka zao hususani utoaji wa haraka wa utabiri wa hali ya hewa.

Vilevile, amewataka kuhakikisha wanabadilishana uzoefu wa namna bora ya kuendesha mamlaka hizo katika kuwahudumia wakulima, wavuvi na wafugaji ambao wanategemea zaidi taarifa za hali ya hewa kwenye shughuli zao za uchumi.

"Mkoa wa Mwanza una zaidi ya wananchi milioni tatu kwa mujibu wa sensa ya hivi karibuni na unashika nafasi ya pili kwenye uchangiaji wa pato la Taifa hivyo wachimbaji wa madini, wakulima na wavuvi ni lazima wapate taarifa sahihi za utabiri wa hali hewa kabla hawajaingia kwenye shughuli zao." RAS Elikana.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwakaribisha washiriki kutembelea vivutio vya utalii kwenye mkoani humo hususani Hifadhi ya Taifa Saanane na kituo cha Bujora na akawakaribisha wawekezaji mkoani humo kwani fursa ni nyingi za kuwekeza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti