Maoni ya Rasimu za kanuni za Sheria ya LATRA yapokelewa Mwanza
Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano kupitia Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini ( LATRA) imekutana na wadau wa usafirishaji jijini Mwanza kwa ajili ya kutoa maoni ya rasimu za kanuni za Sheria ya LATRA.

Akifungua kikao hicho Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Christopher Kadio amewataka wadau hao kutoa maoni yao kwa uwazi ili yaweze kufanyiwa kazi.

"Kuna utaratibu wa kuwa tunalalamika baadaye hivyo tumepewa nafasi hii ili tuitumie kwa umakini sana," amesema.
Ameongeza kuwa jumla ya kanuni nane zitawasilishwa na kupitiwa na wadau hao.

Awali mkurugenzi mkuu wa LATRA Gilliard Ngewe amesema lengo ni kuboresha Mamlaka hiyo ya Udhibiti usafiri Ardhini (LATRA)