• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mapato, uchumi vyaimarika Mwanza

Posted on: March 22nd, 2020

Maendeleo ni mchakato mrefu unaogharimu muda, rasilimali fedha na utaalam.

Kote duniani maendeleo hupimwa katika misingi ya kuimarika na kuboreka kwa huduma za kijamii.

Ili kufikia maendeleo, ni lazima pawepo mikakati madhubuti na endelevu ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya muda mfupi, kati na mrefu.

Tangu ilivyoingia madarakani Novemba 5, 2015, Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imejipambanua kuwa na nia thabiti ya kujenga Tanzania mpya, Tanzania ya watu wanaochapa kazi.

Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake, Rais Magufuli amefanya mengi ya kupigiwa mfano katika maendeleo ya sekta za afya, elimu, maji, usafirishaji, na miundombinu ya barabara.

Kazi zote zimefanyika kutekeleza ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ahadi za Rais Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 pamoja na ahadi au mahitaji mengine yanayotokea katika ziara mbalimbali za viongozi.

Kwa mkoa wa Mwanza, kazi nyingi na kubwa zimefanyika kuhakikisha upatikanaji wa maendeleo endelevu kwa wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela anasema mikakati hiyo ya maendeleo inahusisha mazingira wezeshi kwa wananchi kufanya na kushiriki shughuli za uzalishaji mali kuanzia ngazi ya msingi hadi Taifa.

“Tunapozungumzia Tanzania yenye uchumi wa kati kupitia maendeleo ya sekta ya viwanda ifikapo 2015, tunalenga kumwezesha kila Mtanzania pale alipo kuzalisha, kuuza na kufanya biashara kulingana na mahitaji, mazingira na mtaji wake,” anasema Mongella

Sekta za kilimo, uvuvi, uwekezaji na biashara ni kati ya maeneo muhimu yanayotumiwa na wakazi wa mkoa wa Mwanza kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

Shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazotekelezwa na wakazi wa mkoa huo umewezesha mkoa wa Mwanza kushuhudia ukuaji wa uchumi kwa kwa asilimia 8 huku pato la mkoa likiongezeka kila mwaka.

Mongella anasema kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Pato la Mkoa wa Mwanza limeongezeka kutoka Sh10.05 trilioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh11.3 trilioni mwaka 2017.

Kiwango hicho kimeufanya mkoa wa Mwanza kushika nafasi ya pili baada ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkoa pia umeshika nafasi ya pili Kitaifa kwa kuchangia asilimia 9.79 ya pato la Taifa mwaka 2017 kulinganisha na asilimia 9.69 ya mwaka 2016.

“Wastani wa kipato kwa mwaka kwa kila mwananchi umeongezeka kutoka Sh2.2 milioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh2.3 milioni mwaka 2017.

“Ongezeko la kipato inaimarisha uwezo wa wananchi wa kununua na kuuza; hii inatoa ishara njema kwa uchumi wa mkoa na mtu mmoja mmoja,” anasema Mhe.Mongella.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti