• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA MISUNGWI YAMKOSHA KIONGOZI WA MWENGE

Posted on: August 29th, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Ismail Ali Ussi ameupongeza Uongozi wa Wilaya ya Misungwi kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa matumizi ya Nishati safi ya kupikia ya mwaka 2024 - 2034 kwa kuhamasisha na kutoa Elimu kwa jamii juu ya matumizi sahihi.

Ndugu Ussi Ametoa pongezi hizo leo tarehe 29 Agosti, 2025 katika kijiji cha Iteja wakati Mwenge wa Uhuru ulipofika katika shule ya sekondari ya Aimee Milembe na kukagua matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo imesimikwa miundombinu ya kisasa inayotumia gesi ya asili.

Ndugu Ussi amesema kwa kuelimisha jamii Wilaya hiyo inatelekeza vema na kwa vitendo kampeni ya nishati safi ya kupikia Kitaifa na Kimataifa inayolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kupunguza athari za kimazingira.

Aidha, amebainisha kuwa masuala ya nishati safi ya kupikia pamoja na afua zingine za kukabiliana na athari za kimazingira ni utekeleza wa agenda ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkakati wa kuhakikisha 80%ya watanzania wanatumia nishati safi ifikapo 2034.

Naye, Mkuu wa wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi amesema wilaya hiyo ina vikundi 4 vya wanawake vinavyozalisha wastani wa majiko banifu 200 kwa Mwezi, kaya 11,567 zinazotumia gesi (LPG) kwa ajili ya kupikia, Migahawa 3 na Taasisi 3 za Elimu.

Mhe. Samizi ameongeza kuwa chini ya ushirikiano na mdau wa maendeleo Africa School House wameweza kuokoa gharama ya kupikia kutoka shilingi 500,000 ziizokuwa zikitumuika awali kununua kuni hadi shilingi 300,000 zanazotumika sasa kununua Gesi kwa mwezi.

Kabla ya kukagua matumizi ya nishati safi katika shule hiyo mwenge wa uhuru umezindua klabu ya kupambana na rushwa ambapo wanafunzi wamejipanga kutoa elimu kwa wenzao na jamii kwa ujumla kuhakikisha wanapambana na udhalimu wa matendo ya rushwa ambayo yanaathiri uzalendo na kupelekea ubadhirifu wa mali za umma.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti