• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MELI YA MV. MWANZA YAPOKEA SHEHENA ZA SAMANI

Posted on: March 24th, 2025

MELI YA MV. MWANZA YAPOKEA SHEHENA ZA SAMANI


Leo Machi 24, 2025 Mkuu wa Wilaya  Nyamagana Mhe. Amina Makilagi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ameongoza hafla fupi ya mapokezi ya magari tisa yaliyobeba makasha yenye mzigo wa samani zitakazofungwa kwenye Meli ya Mv. Mwanza inayojengwa katika ziwa Viktoria.

Akizungumza katika mapokezi hayo Mhe. Makilagi amesema kuwasili kwa samani hizo ni hatua muhimu katika kuelekea kukamilisha mradi huo ambao kwa sasa umefikia asilimia 96 ya utekelezaji wake na ambao unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Mei, 2025.

“Hatua hii ya mwisho ni kielelezo tosha ya namna Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyoufungua Mkoa wa Mwanza, unao changia pato la Taifa kwa asilimia 7.2”. Mhe. Makilagi.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameitaka Menejimenti ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) kuhakikisha inasimamia vema mradi huo ili ukamilike kama ulivyopangwa na kufanikisha azma ya Serikali ya kuboresha huduma ya usafiri kwa njia ya maji kwa abiria na mizigo kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa.

“Kukamilika kwa mradi huu kunatarajiwa kuongeza chachu kwa ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na nchi jirani kwa kutoa huduma za usafiri zilizo salama, bora na za uhakika”. Amesema Mhe. Makilagi

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa TASHICO Bi. Amina Mtibampema amesema leo wamepokea vifaa yaani viti vya madaraja yote ambapo mara baada ya kukamilika kwa zoezi la umaliziaji wa meli hiyo kampuni hiyo ya meli itakwenda kufungua uchumi wa Mkoa, wafanyakazi wa TASHICO pamoja na Taifa kiujumla.

“Tutaendelea kusimamia mradi huu kwa maendeleo ya Taifa, na baada ya kupokea Vifaa hivi ufungaji utaanza mara moja”. Bi. Amina.

Mradi huo wa Meli ya Mv. Mwanza kwa sasa umefika asilimia 96 na fedha zilizolipwa hadi sasa ni asilimia 93. Aidha Meli hiyo itakapokamilika itakuwa ndiyo meli kubwa kuliko zote katika Ziwa Viktoria ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo, magari madogo 20 na magari makubwa 3.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti