• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mfuko wa Aga Khan watoa Ruzuku kwa Vikundi vya Wajasiriamali Mwanza

Posted on: June 30th, 2022


Mhe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa rai kwa Vikundi vilivyofuzu kupata ruzuku kwa ajili ya kuendesha biashara katika kupambana na athari zitokanazo na ugonjwa wa Uviko 19 kuzingatia malengo ya mradi ili kufikia malengo.


Amesema hayo mapema leo kwenye Ukumbi wa Nyerere-Gold Crest Hotel wakati wa hafla ya Utoaji Ruzuku ya zaidi ya Tshs Milioni 169 kwa vikundi 90 vya huduma ndogo ya fedha iliyoratibiwa na Shirika la Aga Khan Foundation mradi unaolenga kupambana na athari za Ugonjwa wa Uviko 19 kwa jamii.


"Kipekee kabisa naomba nimshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia awamu ya Sita  ya uongozi wake kwa kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi mbalimbali ikiwemo Umoja wa Ulaya ambao pia wamefadhili mradi huu wakishirikiana na Shirika la Aga Khan Foundation." Mkuu wa Mkoa.

"Hii ni fursa kubwa sana kwa mkoa kwa kupatiwa usaidizi wa kitaalamu na kifedha katika kuhakikisha wananchi wetu wanajengewa uwezo hivyo ni lazima mdhihirishe kwamba kule kuaminiwa kwenu kunaleta taswira kwamba Mwanza mradi ukileta unatekelezeka." Mhandisi Gabriel.

"Naomba niwasihi wanavikundi wote kuwa ruzuku hizi sio kwa ajili ya kufanyia sherehe au kujengea nyumba, mnapewa fedha kwa ajili ya kuendesha biashara zenu katika kujiinua kutoka kwenye umasikini." Simon Meigaro, Kaimu Mkurugenzi Mkazi The Aga Khan Foundation.

Mratibu wa mradi wa utoaji ruzuku kwa vikundi vya huduma ndogo ya fedha, Japhet Wange amesema vikundi vyote vilivyopo kwenye mradi huo vitapata ruzuku ya zaidi ya Milioni 169 na vinaanza rasmi kazi na kwamba mradi upo kwenye mfumo wa hisa ambazo zitaendeshwa kwa kutumia simu katika kufikia malengo.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tuliandaa utaratibu wa kupata vikundi hivi na tunashukuru ofisi za Maafisa maendeleo za Halmashauri na Mkoa kwa usaidizi na hapa leo tupo na vikundi vya wawakilishi 90 ambavyo ndivyo vinaenda kupokea ruzuku hizi," amebainisha Wange.

"Vilevile, Mradi wetu unafanya kazi na vijana wajasiriamali na tunao vijana 100 kutoka kwenye mkoa huu ambao watajengewa uwezo wa kuboresha biashara zao ili waweze kujiinua na kuwaajiri hata vijana wenzao kwenye jamii." amefafanua.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti